📰 HABARI MPYA
Inapakia habari...

OFISI YA MBUNGE KANONI YATOA POLE, YALAANI VITENDO VYA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI MADIBILA

OFISI YA MBUNGE KANONI YATOA POLE, YALAANI VITENDO VYA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI MADIBILA

 

Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni, inatoa pole kwa ndugu, jamaa, marafiki na wananchi wote walioguswa na kifo cha marehemu Daudy Amosi Mwimazi, aliyepoteza maisha katika tukio lililotokea katika Kijiji cha Madibila, Kata ya Mambwekenya, Wilaya ya Kalambo, Mkoa wa Rukwa.

Ofisi ya Mbunge inalaani vikali kitendo cha baadhi ya wananchi kujichukulia sheria mkononi, ikiwemo kuchoma gari lililokuwa limewabeba vijana waliokuwa wakifanya shughuli za kusajili laini za simu za Halotel, pamoja na kumpiga hadi kufariki dunia kijana huyo kwa tuhuma za kutoa sehemu za siri za wanaume, jambo ambalo linapaswa kuchunguzwa na kuthibitishwa na vyombo vya sheria.

Ofisi ya Mbunge inawakumbusha wananchi kuwa hakuna mtu anayepaswa kujichukulia sheria mkononi. Endapo mtu anatuhumiwa kufanya kosa, anapaswa kufikishwa katika vyombo vya sheria ili uchunguzi ufanyike na hatua stahiki za kisheria zichukuliwe.

Wananchi wa Kalambo wanahimizwa kuendelea kudumisha misingi ya upendo, umoja, mshikamano na amani ambayo imekuwa sehemu ya utamaduni wa jamii ya Kalambo. Ni muhimu kuhakikisha kuwa vitendo vya watu wachache haviharibu taswira nzuri ya Kalambo na wananchi wake.

Aidha, Ofisi ya Mbunge inaliomba Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa kina na wa haki ili kubaini wote waliohusika na tukio hilo na kuhakikisha sheria inachukua mkondo wake. Ofisi pia inawasihi wananchi kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa sahihi zitakazosaidia kuwabaini wahusika wote, huku wakihakikisha kuwa raia wasiohusika hawaathiriki.

Kwa kuhitimisha, Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inawaomba wananchi wote kuendelea kudumisha upendo, ushirikiano, mshikamano na amani, pamoja na kushirikiana kupinga vitendo vya kujichukulia sheria mkononi.

Imetolewa na:
Musa Frackison Mzopola
Katibu wa Mbunge, Jimbo la Kalambo

Umemaliza kusoma habari hii? Tupe maoni, mtazamo au swali lako hapa chini.

Comments

MATUKIO KWA NJIA YA PICHA

Inapakia picha...

HABARI MAARUFU

TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA AWAMU YA PILI

  Katika kutekeleza ahadi ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya kutoa shilingi bilioni 200 kwa vijana ndani ya siku 100 baada ya kuingia madarakani, Wizara ya Mifugo na Uvuvi inautangazia umma kuanza kwa Awamu ya Pili ya utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu kwa vijana. Malengo ya mikopo hiyo ni kuwawezesha vijana kupata mitaji ya kuanzisha na kuendeleza biashara ndogo, biashara za kati na kampuni changa ili kujijengea kipato katika Sekta za Mifugo na Uvuvi. Mikopo hiyo itatolewa kwa njia ya vifaa na pembejeo za uzalishaji, ikiwemo ufugaji wa samaki kwa vizimba, ufugaji wa kuku (chotara, mayai na nyama), mbuzi, kondoo na nguruwe, pamoja na boti za kuhudumia vizimba, boti za uvuvi, zana za uvuvi, mifumo ya ubari (cold chain) katika mazao ya uvuvi, mifumo ya kulazisha vifaranga vya samaki, mifumo na vifaa vya uchakataji wa mazao ya uvuvi ikijumuisha makausho ya dagaa na mwani (dryers). Vigezo na maelekezo kwa waombaji ni kama ifuatavyo: i. Baru...

MHE. MBUNGE KANONI ASHIRIKI MAZISHI YA WAATHIRIKA WA AJALI KAZILA, ATOA WITO WA UPENDO, UMOJA NA MSHIKAMANO

  KALAMBO: Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , ameshiriki mazishi ya wananchi wawili waliofariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea katika Kijiji cha Kazila, Kata ya Mwazye, Wilaya ya Kalambo, huku akitoa pole na faraja kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki pamoja na wananchi wote walioguswa na msiba huo. Ajali hiyo ilitokea tarehe 05 Agosti 2026 , wakati gari aina ya Fuso lililokuwa limebeba watu waliokuwa wakielekea kwenye shughuli ya harusi kutoka Kijiji cha Msoma, Kata ya Mwazye, Wilaya ya Kalambo , lilipofika katika Kijiji cha Kazila kwa ajili ya shughuli ya kufunga ndoa. Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa, gari hilo lilikuwa limembeba bwana harusi, Hosea Gilbert Watua , pamoja na watu wengine waliokuwa wakisafiri naye kutoka Kijiji cha Msoma kuelekea Kijiji cha Kazila, ambako alikuwa akienda kufunga ndoa na bibi harusi, Mehili Sauli Visent , mkazi wa Kijiji cha Kazila, Kata ya Mwazye. AJALI YATOKEA KABLA YA KUFIKA KWENYE DARAJA Taarifa zinaeleza ...