📰 HABARI MPYA
Inapakia habari...

Utalii

Utalii

 Karibu kutembelea Wilaya ya Kalambo, moja ya maeneo yenye vivutio vya utalii nchini Tanzania. Wilaya hii imebarikiwa kuwa na mandhari ya kuvutia, urithi wa asili, tamaduni mbalimbali pamoja na vivutio vinavyowavutia wageni kutoka ndani na nje ya nchi.

Tunakuomba uchunguze na kujionea uzuri wa vivutio vya utalii vinavyopatikana Kalambo, ikiwa ni pamoja na Maporomoko ya Mto Kalambo, maeneo ya kihistoria, fukwe za Ziwa Tanganyika, na mazingira ya asili yenye kuvutia yanayofanya wilaya hii kuwa sehemu maalum ya kutembelea.

Karibu ujionee uzuri wa Kalambo, ugundue historia yake, ufurahie utamaduni wa wakazi wake, na ushiriki katika safari ya kuutangaza utalii wa wilaya yetu ya maendeleo ya jamii kwa ujumla.

Kalambo – Fahari ya Utalii, Historia na Ustawi.


Ziwa Tanganyika

Ziwa Tanganyika ni moja ya maziwa makubwa ya Afrika ya Kati likienea mpakani mwa Tanzania , Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo , Burundi na Zambia .

Ni ziwa kubwa la pili duniani kwa wingi wa maji matamu baada ya Ziwa Baikal ( Siberia ) kwa kuzingatia kiasi cha maji ndani yake na kina (hadi mita 1,470).

Kwa eneo lake ( km² 32,893) ni la pili tu baada ya Viktoria Nyanza katika Afrika .

Maji yake hutoka kuelekea mto Kongo hatimaye katika Bahari Atlantiki .

Mili ya Mv Liemba


MV Liemba (MV kwa Kiing. motor chombo ) ni meli ya Ki tanzania inayohudumia pwani za Ziwa Tanganyika . Ni chombo cha usafiri kwa maji chenye umri mkubwa kipo tangu mwaka 1914. Meli inasukumwa na injini ya diseli na urefu wake ni mita 67, upana mita 10 na ukubwa unatajwa ama kuwa tani 1500 au 1200. Ina ya kubeba abiria hadi 600 pamoja na mzigo tani 200 kati ya mabandari ya Ziwa Tanganyika JPM upande wa Tanzania ( Zambia ) upande wa Tanzania K. na Bujumbura ( Burundi ).

Samaki wa Mapambo ziwa Tanganyika

Ziwa Tanganyika ni hifadhi kubwa ya kibiolojia zaidi ya aina 200 za samaki wa mapambo,hasa kutoka kwa familia ya Cichlidae , ambao wanathaminiwa sana katika soko la kimataifa la vifaa vya kufuga samaki. Samaki hawa wa thamani huvuliwa kibiashara na kusafirisha kwenda nchi za nje.

Maporomoko ya Kalambo Falls

Maporomoko ya Kalambo yanatokana na mto Kalambo ambao ni mpaka wa Tanzania na Zambia .

Maporomoko ya maji hayo ya mita 235 kwa mkupuo mmoja, ukiachilia kuwa ni ya pili baada ya yale ya Tugela ( Afrika ya Kusini ), lakini pia ndiyo maporomoko pekee yanayogawa nchi mbili.

Maporomoko hayo yapo katika kijiji cha Kapozwa, kata ya Kisumba , Wilaya ya Kalambo , Mkoa wa Rukwa . Katika kijiji cha Kapozwa, ambacho kinatokana na imani kuwa ukienda kuoga katika maporomoko hayo utapooza. Kwa kuambiwa hivyo wenyeji wa eneo hilo walipaita jina la Kapozwa.

Maporomoko hayo yamekuwa yakionekana na kutangazwa kuwa yapo Zambia na hivyo kuiondoa Tanzania miongoni mwa nchi zenye maporomoko yanayotambulika duniani .

Chemichemi ya Maji yanayo Chemka

Chemichemi hii ya maji yanayo chemka ipo kijiji cha Kizombwe kata ya Mkali wilaya ya Kalambo haya ni maji ya ajabu mda wote yana chemka ni maji yanayo unguza ukigusa ukifika Kalambo maji yalipo ni kilometa 8 kutoka makao mkuu ya wilaya kwenye mji wa Matai.

MATUKIO KWA NJIA YA PICHA

Inapakia picha...

HABARI MAARUFU

ZIARA YA MHE. KANONI KATIKA JIMBO LA KALAMBO IMEAIRISHWA; HIKI NDICHO KILICHOSABABISHA.

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo na umma kwa ujumla kuwa ziara iliyokuwa imepangwa kufanyika kuanzia tarehe 20 Julai 2026 hadi tarehe 10 Agosti 2026 imeahirishwa. Uamuzi huo umetokana na zuio la Serikali kuhusu kufanyika kwa mikutano ya hadhara katika kipindi hiki. Ofisi ya Mbunge inaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza na inaendelea kuwashukuru wananchi kwa ushirikiano na uelewa wao. Kwa taarifa zaidi na maendeleo ya shughuli za Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, tembelea: www.mbungekalambo.com Imetolewa na: Musa Frackison Mzopola Katibu wa Mbunge, Jimbo la Kalambo

HATIMAYE! ORODHA RASMI YA WANUFAIKA WA MIKOPO YA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI KWA WILAYA YA KALAMBO YATOLEWA – WANUFAIKA WOTE WATAKIWA KUHUDHURIA MAFUNZO MUHIMU

  TAARIFA KWA UMMA Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwajulisha wananchi wote wa Wilaya ya Kalambo kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekamilisha mapitio ya maombi ya mikopo yaliyowasilishwa na wananchi wa Wilaya ya Kalambo kupitia programu ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi. Kutokana na mchakato huo, Wizara imetoa rasmi orodha ya wanufaika waliokidhi vigezo na kufanikiwa kupata mikopo hiyo. Wanufaika kutoka Wilaya ya Kalambo ni kama ilivyoainishwa katika orodha rasmi ya Wizara, ambayo inajumuisha: Rahel John Mawela – Mradi wa Mbuzi Faustina Cladio Msumeno – Mradi wa Kuku wa Mayai William Isaya Moringe – Mradi wa Mbuzi Mashaka Medard Jastin – Mradi wa Mfumo wa Ubaridi Aibini Leonard John – Mradi wa Mbuzi Britney Shadi Pandisha – Mradi wa Kuku wa Nyama Sisilia Augustino Michael – Mradi wa Mbuzi Ofisi ya Mbunge inawapongeza wanufaika wote kwa kufanikiwa kupata fursa hiyo muhimu na inawatakia mafanikio katika utekelezaji wa ...

ZIARA YA MIKUTANO YA HADHARA YA MHE. EDEFONSI JOACKIM KANONI MBUNGE JIMBO LA KALAMBO YATANGAZWA

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo kuwa Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni (Mb), Mbunge wa Jimbo la Kalambo, atafanya ziara ya mikutano ya hadhara katika kata na vijiji mbalimbali vya jimbo kuanzia tarehe 20 Julai, 2026 hadi tarehe 10 Agosti, 2026, kwa mujibu wa ratiba iliyoambatanishwa.    Ziara hii inalenga kuimarisha mawasiliano kati ya Mbunge na wananchi kwa kukutana nao ana kwa ana, kusikiliza maoni, kero na changamoto zinazowakabili, pamoja na kupokea mapendekezo yatakayosaidia kuboresha huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo ya Jimbo la Kalambo. Aidha, Mhe. Mbunge atatoa mrejesho kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kueleza mipango ya maendeleo inayotarajiwa kutekelezwa katika maeneo mbalimbali ya jimbo. Wananchi watapata fursa ya kuuliza maswali, kutoa maoni yao na kushiriki katika kujadili masuala muhimu yanayohusu maendeleo ya kata na vijiji vyao. Ushiriki wa wananchi katika mikutano hii ni msingi m...