Karibu kutembelea Wilaya ya Kalambo, moja ya maeneo yenye vivutio vya utalii nchini Tanzania. Wilaya hii imebarikiwa kuwa na mandhari ya kuvutia, urithi wa asili, tamaduni mbalimbali pamoja na vivutio vinavyowavutia wageni kutoka ndani na nje ya nchi.
Tunakuomba uchunguze na kujionea uzuri wa vivutio vya utalii vinavyopatikana Kalambo, ikiwa ni pamoja na Maporomoko ya Mto Kalambo, maeneo ya kihistoria, fukwe za Ziwa Tanganyika, na mazingira ya asili yenye kuvutia yanayofanya wilaya hii kuwa sehemu maalum ya kutembelea.
Karibu ujionee uzuri wa Kalambo, ugundue historia yake, ufurahie utamaduni wa wakazi wake, na ushiriki katika safari ya kuutangaza utalii wa wilaya yetu ya maendeleo ya jamii kwa ujumla.
Kalambo – Fahari ya Utalii, Historia na Ustawi.
Ziwa Tanganyika ni moja ya maziwa makubwa ya Afrika ya Kati likienea mpakani mwa Tanzania , Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo , Burundi na Zambia .
Ni ziwa kubwa la pili duniani kwa wingi wa maji matamu baada ya Ziwa Baikal ( Siberia ) kwa kuzingatia kiasi cha maji ndani yake na kina (hadi mita 1,470).
Kwa eneo lake ( km² 32,893) ni la pili tu baada ya Viktoria Nyanza katika Afrika .
Maji yake hutoka kuelekea mto Kongo hatimaye katika Bahari Atlantiki .

Mili ya Mv Liemba
MV Liemba (MV kwa Kiing. motor chombo ) ni meli ya Ki tanzania inayohudumia pwani za Ziwa Tanganyika . Ni chombo cha usafiri kwa maji chenye umri mkubwa kipo tangu mwaka 1914. Meli inasukumwa na injini ya diseli na urefu wake ni mita 67, upana mita 10 na ukubwa unatajwa ama kuwa tani 1500 au 1200. Ina ya kubeba abiria hadi 600 pamoja na mzigo tani 200 kati ya mabandari ya Ziwa Tanganyika JPM upande wa Tanzania ( Zambia ) upande wa Tanzania K. na Bujumbura ( Burundi ).

Samaki wa Mapambo ziwa Tanganyika
Ziwa Tanganyika ni hifadhi kubwa ya kibiolojia zaidi ya aina 200 za samaki wa mapambo,hasa kutoka kwa familia ya Cichlidae , ambao wanathaminiwa sana katika soko la kimataifa la vifaa vya kufuga samaki. Samaki hawa wa thamani huvuliwa kibiashara na kusafirisha kwenda nchi za nje.
Maporomoko ya Kalambo yanatokana na mto Kalambo ambao ni mpaka wa Tanzania na Zambia .
Maporomoko ya maji hayo ya mita 235 kwa mkupuo mmoja, ukiachilia kuwa ni ya pili baada ya yale ya Tugela ( Afrika ya Kusini ), lakini pia ndiyo maporomoko pekee yanayogawa nchi mbili.
Maporomoko hayo yapo katika kijiji cha Kapozwa, kata ya Kisumba , Wilaya ya Kalambo , Mkoa wa Rukwa . Katika kijiji cha Kapozwa, ambacho kinatokana na imani kuwa ukienda kuoga katika maporomoko hayo utapooza. Kwa kuambiwa hivyo wenyeji wa eneo hilo walipaita jina la Kapozwa.
Maporomoko hayo yamekuwa yakionekana na kutangazwa kuwa yapo Zambia na hivyo kuiondoa Tanzania miongoni mwa nchi zenye maporomoko yanayotambulika duniani .

Chemichemi ya Maji yanayo Chemka
Chemichemi hii ya maji yanayo chemka ipo kijiji cha Kizombwe kata ya Mkali wilaya ya Kalambo haya ni maji ya ajabu mda wote yana chemka ni maji yanayo unguza ukigusa ukifika Kalambo maji yalipo ni kilometa 8 kutoka makao mkuu ya wilaya kwenye mji wa Matai.


