📰 HABARI MPYA
Inapakia habari...

NAFASI 200 ZA AJIRA ZA MAFUNDI ZATANGAZWA KWA KAZI NCHINI SAUDI ARABIA

NAFASI 200 ZA AJIRA ZA MAFUNDI ZATANGAZWA KWA KAZI NCHINI SAUDI ARABIA

 

Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, kwa kushirikiana na Atilis Investment Limited, inawataarifu Watanzania wenye sifa stahiki kuhusu nafasi 200 za ajira za mafundi katika sekta ya ujenzi, zilizotolewa na kampuni ya Shade Corporation Limited ya nchini Saudi Arabia.

KADA ZINAZOHITAJIKA

Nafasi hizo zinahusisha mafundi wa kada mbalimbali, wakiwemo:

  • Mafundi Uashi
  • Mafundi Useremala
  • Wasuka Nondo

SIFA ZA MWOMBAJI

Mwombaji anatakiwa kuwa na:

  • Elimu ya astashahada kutoka chuo cha ufundi kinachotambuliwa na Serikali;
  • Uzoefu wa kazi wa miaka miwili (2) au zaidi katika sekta ya ufundi;
  • Uwezo na uzoefu katika kada husika, ikiwemo Uashi, Useremala au Usuka Nondo;
  • Umri kati ya miaka 21 hadi 40;
  • Waombaji wa nafasi hizi wanatakiwa kuwa wanaume.

MASHARTI NA MAFANO YA AJIRA

Waombaji watakaofaulu mchakato wa ajira watapata fursa ya kufanya kazi nchini Saudi Arabia kwa masharti yaliyowekwa na mwajiri.

Miongoni mwa mafao na masharti ya ajira ni:

  • Mshahara wa Riyal 1,100 za Saudi Arabia kwa mwezi;
  • Posho ya chakula ya Riyal 275 kwa mwezi;
  • Mwajiri kugharamia matibabu katika kipindi chote cha ajira;
  • Mwajiri kugharamia usafiri kutoka eneo la makazi ya mfanyakazi hadi kituo cha kazi katika kipindi cha ajira;
  • Mwajiri kugharamia tiketi ya ndege ya kwenda Saudi Arabia na kurudi baada ya mkataba kuisha;
  • Mwajiri kugharamia malazi katika kipindi chote cha ajira.

Mkataba wa ajira utakuwa wa miezi sita (6) na unaweza kuhuishwa kwa makubaliano na masharti ya mwajiri.

JINSI YA KUTUMA MAOMBI

Waombaji wanatakiwa kutuma CV pamoja na nakala za vyeti vya taaluma kupitia barua pepe:

[email protected]

Baada ya kutuma maombi, mwombaji anatakiwa pia kujisajili kupitia mfumo wa ajira wa Serikali:

jobs.kazi.go.tz

Mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 30 Agosti 2026.

TAREHE NA ENEO LA USAILI

Usaili utafanyika tarehe:

31 Agosti 2026 na 1 Septemba 2026

Eneo:
Itumbi Hotel – Ghorofa ya 5, Magomeni Mwembechai, Dar es Salaam.

MAWASILIANO

Kwa maelezo zaidi, waombaji wanaweza kuwasiliana kupitia:

Simu:
+255 711 707 500
+255 781 182 914

Tovuti:
jobs.kazi.go.tz

Tangazo hili limetolewa kwa ushirikiano na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, likiwa na lengo la kuwawezesha Watanzania wenye sifa kupata fursa za ajira katika sekta ya ujenzi nchini Saudi Arabia.

TAARIFA KWA WAKAZI WA WILAYA YA KALAMBO

Kwa waombaji kutoka Wilaya ya Kalambo wanaotuma maombi ya nafasi hizi, wanashauriwa kutoa taarifa kwa Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo ili Ofisi iwe na taarifa za waombaji kutoka Jimbo la Kalambo na iweze kusaidia katika ufuatiliaji wa mchakato pale inapohitajika.

Mawasiliano ya Ofisi ya Mbunge Jimbo la Kalambo

Simu: 0625850656
Barua pepe: [email protected]
Tovuti: www.mbungekalambo.com




Umemaliza kusoma habari hii? Tupe maoni, mtazamo au swali lako hapa chini.

Comments

MATUKIO KWA NJIA YA PICHA

Inapakia picha...

HABARI MAARUFU

TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA AWAMU YA PILI

  Katika kutekeleza ahadi ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya kutoa shilingi bilioni 200 kwa vijana ndani ya siku 100 baada ya kuingia madarakani, Wizara ya Mifugo na Uvuvi inautangazia umma kuanza kwa Awamu ya Pili ya utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu kwa vijana. Malengo ya mikopo hiyo ni kuwawezesha vijana kupata mitaji ya kuanzisha na kuendeleza biashara ndogo, biashara za kati na kampuni changa ili kujijengea kipato katika Sekta za Mifugo na Uvuvi. Mikopo hiyo itatolewa kwa njia ya vifaa na pembejeo za uzalishaji, ikiwemo ufugaji wa samaki kwa vizimba, ufugaji wa kuku (chotara, mayai na nyama), mbuzi, kondoo na nguruwe, pamoja na boti za kuhudumia vizimba, boti za uvuvi, zana za uvuvi, mifumo ya ubari (cold chain) katika mazao ya uvuvi, mifumo ya kulazisha vifaranga vya samaki, mifumo na vifaa vya uchakataji wa mazao ya uvuvi ikijumuisha makausho ya dagaa na mwani (dryers). Vigezo na maelekezo kwa waombaji ni kama ifuatavyo: i. Baru...

MHE. MBUNGE KANONI ASHIRIKI MAZISHI YA WAATHIRIKA WA AJALI KAZILA, ATOA WITO WA UPENDO, UMOJA NA MSHIKAMANO

  KALAMBO: Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , ameshiriki mazishi ya wananchi wawili waliofariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea katika Kijiji cha Kazila, Kata ya Mwazye, Wilaya ya Kalambo, huku akitoa pole na faraja kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki pamoja na wananchi wote walioguswa na msiba huo. Ajali hiyo ilitokea tarehe 05 Agosti 2026 , wakati gari aina ya Fuso lililokuwa limebeba watu waliokuwa wakielekea kwenye shughuli ya harusi kutoka Kijiji cha Msoma, Kata ya Mwazye, Wilaya ya Kalambo , lilipofika katika Kijiji cha Kazila kwa ajili ya shughuli ya kufunga ndoa. Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa, gari hilo lilikuwa limembeba bwana harusi, Hosea Gilbert Watua , pamoja na watu wengine waliokuwa wakisafiri naye kutoka Kijiji cha Msoma kuelekea Kijiji cha Kazila, ambako alikuwa akienda kufunga ndoa na bibi harusi, Mehili Sauli Visent , mkazi wa Kijiji cha Kazila, Kata ya Mwazye. AJALI YATOKEA KABLA YA KUFIKA KWENYE DARAJA Taarifa zinaeleza ...