Uongozi wa Ofisi ya Mbunge Jimbo la Kalambo Mkoa wa Rukwa
![]() |
| Mhe: Edifonsi Joackim Kanoni Mbunge Jimbo La Kalambo |
Ndg: Musa Frackison Mzopola
Katibu Mkuu
Simu: 0625850656
Ndg: Joshua Chole
Katibu Msaidizi
Simu: 0783752940
Ofisi ipo Matai B kata ya Lyowa Barabara ya kwenda Ofisi kwa Mkurugenzi Halmashauri mkabala na Ofisi ya TANESCO
Dhamira (Mission)
Kutoa taarifa sahihi, za kuaminika na kwa wakati kuhusu shughuli, miradi ya maendeleo, huduma kwa wananchi na kazi za Mbunge wa Jimbo la Kalambo. Tovuti inalenga kuimarisha uwazi, kuwahusisha wananchi katika maendeleo na kuwa daraja la mawasiliano kati ya Ofisi ya Mbunge na wananchi wa Jimbo la Kalambo.
Mbunge Kalambo
Dira (Vision)
Kuwa jukwaa bora la kidijitali linaloongoza katika utoaji wa taarifa za maendeleo, uwazi na ushirikishwaji wa wananchi, kwa lengo la kujenga Jimbo la Kalambo lenye maendeleo endelevu na huduma bora kwa wananchi wake.
Historia ya Tovuti
Tovuti ya Mbunge Kalambo ilianzishwa kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa taarifa rasmi za Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo. Kupitia tovuti hii, wananchi hupata habari za maendeleo, miradi inayotekelezwa, taarifa rasmi, matangazo, picha, video pamoja na huduma mbalimbali za mawasiliano. Aidha, tovuti imeboreshwa ili iweze kutumika kwa urahisi kupitia simu na kompyuta, na kuwa chanzo cha taarifa sahihi kwa wananchi wa Jimbo la Kalambo na wadau wengine.
Mbunge Kalambo
Timu ya Wahariri
Mhariri Mkuu
Musa Frackison Mzopola
Katibu Mkuu wa Mbunge wa Jimbo la Kalambo
Anasimamia uandaaji, uhakiki na uchapishaji wa habari, taarifa rasmi, matangazo na maudhui yote yanayowekwa kwenye tovuti ya Mbunge Kalambo. Pia anahakikisha taarifa zote zinazingatia usahihi, uwazi na maslahi ya wananchi wa Jimbo la Kalambo.



