📰 HABARI MPYA
Inapakia habari...

Kuhusu Sisi

Kuhusu Sisi

KUHUSU SISI

Karibu MBUNGEKALAMBO.COM, tovuti ya Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inayolenga kuwafikishia wananchi taarifa, habari, shughuli na maendeleo ya Jimbo la Kalambo.

Ofisi ya Mbunge Jimbo la Kalambo

Ofisi ya Mbunge Jimbo la Kalambo inalenga kuimarisha mawasiliano, uwazi na ushirikishwaji wa wananchi katika shughuli mbalimbali za maendeleo ya Jimbo.

Kupitia MBUNGEKALAMBO.COM, wananchi na wadau wanaweza kupata taarifa kuhusu shughuli za Mbunge, maendeleo ya Jimbo, habari, picha, video na taarifa nyingine muhimu.

UONGOZI WA OFISI

Viongozi wa Ofisi ya Mbunge Jimbo la Kalambo

Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni
MBUNGE JIMBO LA KALAMBO

Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni

Mbunge wa Jimbo la Kalambo

Mkoa wa Rukwa

TIMU YA OFISI

Watendaji wa Ofisi ya Mbunge Jimbo la Kalambo

Ndugu Musa Frackison Mzopola

Ndugu Musa Frackison Mzopola

Katibu Mkuu

Ndugu Joshua Chole

Ndugu Joshua Chole

Katibu Msaidizi

Dhamira

Kutoa taarifa sahihi, za kuaminika na kwa wakati kuhusu shughuli, miradi ya maendeleo, huduma kwa wananchi na kazi za Ofisi ya Mbunge Jimbo la Kalambo.

Dira

Kuwa jukwaa bora la kidijitali katika kutoa taarifa, kuimarisha mawasiliano na kuongeza ushirikishwaji wa wananchi katika maendeleo ya Jimbo la Kalambo.

🕒 SAA ZA KAZI ZA OFISI

Ofisi inapatikana kwa huduma wakati wa siku za kazi:

Jumatatu – Ijumaa Saa 3:00 Asubuhi – Saa 10:00 Jioni

Kwa mawasiliano nje ya muda huo, unaweza kutumia njia za mawasiliano zinazopatikana kwenye tovuti.

WASILIANA NA OFISI

Kwa taarifa, maoni, ushauri au mawasiliano na Ofisi ya Mbunge Jimbo la Kalambo.

📞 PIGA SIMU 💬 WHATSAPP ✉️ EMAIL

MATUKIO KWA NJIA YA PICHA

Inapakia picha...

HABARI MAARUFU

FURSA ZA MIKOPO YA VIJANA SASA HADHARANI OMBA SASA UJIKWAMUE KIUCHUMI

  Katika kutekeleza ahadi ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya kutoa shilingi bilioni 200 kwa vijana ndani ya siku 100 baada ya kuingia madarakani, Wizara ya Mifugo na Uvuvi inautangazia umma kuanza kwa Awamu ya Pili ya utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu kwa vijana. Malengo ya mikopo hiyo ni kuwawezesha vijana kupata mitaji ya kuanzisha na kuendeleza biashara ndogo, biashara za kati na kampuni changa ili kujijengea kipato katika Sekta za Mifugo na Uvuvi. Mikopo hiyo itatolewa kwa njia ya vifaa na pembejeo za uzalishaji, ikiwemo ufugaji wa samaki kwa vizimba, ufugaji wa kuku (chotara, mayai na nyama), mbuzi, kondoo na nguruwe, pamoja na boti za kuhudumia vizimba, boti za uvuvi, zana za uvuvi, mifumo ya ubari (cold chain) katika mazao ya uvuvi, mifumo ya kulazisha vifaranga vya samaki, mifumo na vifaa vya uchakataji wa mazao ya uvuvi ikijumuisha makausho ya dagaa na mwani (dryers). Vigezo na maelekezo kwa waombaji ni kama ifuatavyo: i. Baru...

NAFASI 200 ZA AJIRA ZA MAFUNDI ZATANGAZWA KWA KAZI NCHINI SAUDI ARABIA

  Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, kwa kushirikiana na Atilis Investment Limited , inawataarifu Watanzania wenye sifa stahiki kuhusu nafasi 200 za ajira za mafundi katika sekta ya ujenzi , zilizotolewa na kampuni ya Shade Corporation Limited ya nchini Saudi Arabia. KADA ZINAZOHITAJIKA Nafasi hizo zinahusisha mafundi wa kada mbalimbali, wakiwemo: Mafundi Uashi Mafundi Useremala Wasuka Nondo SIFA ZA MWOMBAJI Mwombaji anatakiwa kuwa na: Elimu ya astashahada kutoka chuo cha ufundi kinachotambuliwa na Serikali; Uzoefu wa kazi wa miaka miwili (2) au zaidi katika sekta ya ufundi; Uwezo na uzoefu katika kada husika, ikiwemo Uashi, Useremala au Usuka Nondo; Umri kati ya miaka 21 hadi 40 ; Waombaji wa nafasi hizi wanatakiwa kuwa wanaume . MASHARTI NA MAFANO YA AJIRA Waombaji watakaofaulu mchakato wa ajira watapata fursa ya kufanya kazi nchini Saudi Arabia kwa masharti yaliyowekwa na mwajiri. Miongoni mwa mafao na masharti ya ajira ni: Mshahara wa Riyal 1...

MHE. MBUNGE KANONI ASHIRIKI MAZISHI YA WAATHIRIKA WA AJALI KAZILA, ATOA WITO WA UPENDO, UMOJA NA MSHIKAMANO

  KALAMBO: Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , ameshiriki mazishi ya wananchi wawili waliofariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea katika Kijiji cha Kazila, Kata ya Mwazye, Wilaya ya Kalambo, huku akitoa pole na faraja kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki pamoja na wananchi wote walioguswa na msiba huo. Ajali hiyo ilitokea tarehe 05 Agosti 2026 , wakati gari aina ya Fuso lililokuwa limebeba watu waliokuwa wakielekea kwenye shughuli ya harusi kutoka Kijiji cha Msoma, Kata ya Mwazye, Wilaya ya Kalambo , lilipofika katika Kijiji cha Kazila kwa ajili ya shughuli ya kufunga ndoa. Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa, gari hilo lilikuwa limembeba bwana harusi, Hosea Gilbert Watua , pamoja na watu wengine waliokuwa wakisafiri naye kutoka Kijiji cha Msoma kuelekea Kijiji cha Kazila, ambako alikuwa akienda kufunga ndoa na bibi harusi, Mehili Sauli Visent , mkazi wa Kijiji cha Kazila, Kata ya Mwazye. AJALI YATOKEA KABLA YA KUFIKA KWENYE DARAJA Taarifa zinaeleza ...