Wilaya ya Kalambo
Wilaya ya Kalambo ni wilaya mpya katika mkoa wa Rukwa yenye postikodi namba 55400 , ambayo imeandikwa rasmi mnamo Machi 2012 . Makao makuu ya wilaya yako Matai . Mkuu wa wilaya ya kwanza alikuwa Moshi Chang'a . Wilaya limepokea jina kutoka kwa mto Kalambo unaopita hapa hadi kuishia kweye Maporomoko ya Kalambo upande wa Zambia . Idadi ya wakazi wa wilaya ilikuwa 207,700 wakati wa mwaka wa 2012. Katika mwaka wa 2022 walihesabiwa 316,783 Kata za wilaya ya Kalambo katika Kanyezi | Kasanga | Katazi | Kate | Kilesha | Kisumba | Legezamwendo | Lyowa | Mambwekenya | Mambwe Nkoswe | Matai | Mbuluma | Mkali | Mkowe | Mnamba | Mpombwe | Msanzi | Mwazye | Mwimbi | Samazi | Sopa | Sundu | Ulumi .
Takwimu
- Idadi ya Wananchi wilaya ya Kalambo Sensa 2022
- Jumla kuu 316783
- Wanaume 153124.
- Wanawake 163659.
- Kata 23
- Vijiji 111
- Vitongoji 422
- Kaya 69225.

