Mhe. Kanoni amesema kuwa ahadi yake ya kuhakikisha ndani ya kipindi cha miaka mitano Kata za Mambwe zinapata gari la kubebea wagonjwa (Ambulensi) sasa imetimia, baada ya gari hilo kupatikana rasmi.
Gari la kubebea wagonjwa (ambulensi) litakabidhiwa rasmi na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Mhe. Prof. Riziki Silas Shemdoe (Mb.), tarehe 10 Julai 2026.na itaanza kutumika katika Kituo cha Afya Legezamwendo, kilichopo Kata ya Legezamwendo.
Kupatikana kwa gari hilo kutarahisisha kwa kiasi kikubwa huduma za afya kwa wananchi wa Kata za Mambwe, ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya usafiri wa kuwapeleka wagonjwa katika vituo vya afya na hospitali kwa ajili ya matibabu ya dharura.
Mhe. Kanoni ametoa shukrani zake za dhati kwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Mawaziri, viongozi na watendaji wote wa Serikali kwa ushirikiano wanaoendelea kumpatia katika kuwaletea maendeleo wananchi wa Kalambo na Watanzania kwa ujumla.
Aidha, amewataka wananchi wa Kalambo kuendelea kudumisha amani, upendo na mshikamano, ili kushirikiana katika kuijenga Kalambo yenye maendeleo endelevu na ustawi wa wananchi wake.
KALAMBO – KAZI NA UTU, TUNASONGA MBELE
MAENDELEO KWA VITENDO
Imetolewa na:
Musa Frackison Mzopola
Katibu wa Mbunge
Jimbo la Kalambo

