📰 HABARI MPYA
Inapakia habari...

MHE. EDIFONSI JOACKIM KANONI ATEKELEZA AHADI YAKE YA KULETA GARI LA WAGONJWA KATA ZA MAMBWE

MHE. EDIFONSI JOACKIM KANONI ATEKELEZA AHADI YAKE YA KULETA GARI LA WAGONJWA KATA ZA MAMBWE

 




Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edifonsi Joackim Kanoni, ameendelea kutekeleza ahadi alizozitoa kwa wananchi kupitia Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2025–2030, kwa kuhakikisha huduma za afya zinaimarishwa katika Jimbo la Kalambo.

Mhe. Kanoni amesema kuwa ahadi yake ya kuhakikisha ndani ya kipindi cha miaka mitano Kata za Mambwe zinapata gari la kubebea wagonjwa (Ambulensi) sasa imetimia, baada ya gari hilo kupatikana rasmi.

Gari la kubebea wagonjwa (ambulensi) litakabidhiwa rasmi na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Mhe. Prof. Riziki Silas Shemdoe (Mb.), tarehe 10 Julai 2026.na itaanza kutumika katika Kituo cha Afya Legezamwendo, kilichopo Kata ya Legezamwendo.

Kupatikana kwa gari hilo kutarahisisha kwa kiasi kikubwa huduma za afya kwa wananchi wa Kata za Mambwe, ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya usafiri wa kuwapeleka wagonjwa katika vituo vya afya na hospitali kwa ajili ya matibabu ya dharura.

Mhe. Kanoni ametoa shukrani zake za dhati kwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Mawaziri, viongozi na watendaji wote wa Serikali kwa ushirikiano wanaoendelea kumpatia katika kuwaletea maendeleo wananchi wa Kalambo na Watanzania kwa ujumla.

Aidha, amewataka wananchi wa Kalambo kuendelea kudumisha amani, upendo na mshikamano, ili kushirikiana katika kuijenga Kalambo yenye maendeleo endelevu na ustawi wa wananchi wake.

KALAMBO – KAZI NA UTU, TUNASONGA MBELE

MAENDELEO KWA VITENDO

Imetolewa na:

Musa Frackison Mzopola
Katibu wa Mbunge
Jimbo la Kalambo

MATUKIO KWA NJIA YA PICHA

Inapakia picha...

HABARI MAARUFU

ZIARA YA MHE. KANONI KATIKA JIMBO LA KALAMBO IMEAIRISHWA; HIKI NDICHO KILICHOSABABISHA.

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo na umma kwa ujumla kuwa ziara iliyokuwa imepangwa kufanyika kuanzia tarehe 20 Julai 2026 hadi tarehe 10 Agosti 2026 imeahirishwa. Uamuzi huo umetokana na zuio la Serikali kuhusu kufanyika kwa mikutano ya hadhara katika kipindi hiki. Ofisi ya Mbunge inaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza na inaendelea kuwashukuru wananchi kwa ushirikiano na uelewa wao. Kwa taarifa zaidi na maendeleo ya shughuli za Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, tembelea: www.mbungekalambo.com Imetolewa na: Musa Frackison Mzopola Katibu wa Mbunge, Jimbo la Kalambo

HATIMAYE! ORODHA RASMI YA WANUFAIKA WA MIKOPO YA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI KWA WILAYA YA KALAMBO YATOLEWA – WANUFAIKA WOTE WATAKIWA KUHUDHURIA MAFUNZO MUHIMU

  TAARIFA KWA UMMA Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwajulisha wananchi wote wa Wilaya ya Kalambo kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekamilisha mapitio ya maombi ya mikopo yaliyowasilishwa na wananchi wa Wilaya ya Kalambo kupitia programu ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi. Kutokana na mchakato huo, Wizara imetoa rasmi orodha ya wanufaika waliokidhi vigezo na kufanikiwa kupata mikopo hiyo. Wanufaika kutoka Wilaya ya Kalambo ni kama ilivyoainishwa katika orodha rasmi ya Wizara, ambayo inajumuisha: Rahel John Mawela – Mradi wa Mbuzi Faustina Cladio Msumeno – Mradi wa Kuku wa Mayai William Isaya Moringe – Mradi wa Mbuzi Mashaka Medard Jastin – Mradi wa Mfumo wa Ubaridi Aibini Leonard John – Mradi wa Mbuzi Britney Shadi Pandisha – Mradi wa Kuku wa Nyama Sisilia Augustino Michael – Mradi wa Mbuzi Ofisi ya Mbunge inawapongeza wanufaika wote kwa kufanikiwa kupata fursa hiyo muhimu na inawatakia mafanikio katika utekelezaji wa ...

ZIARA YA MIKUTANO YA HADHARA YA MHE. EDEFONSI JOACKIM KANONI MBUNGE JIMBO LA KALAMBO YATANGAZWA

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo kuwa Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni (Mb), Mbunge wa Jimbo la Kalambo, atafanya ziara ya mikutano ya hadhara katika kata na vijiji mbalimbali vya jimbo kuanzia tarehe 20 Julai, 2026 hadi tarehe 10 Agosti, 2026, kwa mujibu wa ratiba iliyoambatanishwa.    Ziara hii inalenga kuimarisha mawasiliano kati ya Mbunge na wananchi kwa kukutana nao ana kwa ana, kusikiliza maoni, kero na changamoto zinazowakabili, pamoja na kupokea mapendekezo yatakayosaidia kuboresha huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo ya Jimbo la Kalambo. Aidha, Mhe. Mbunge atatoa mrejesho kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kueleza mipango ya maendeleo inayotarajiwa kutekelezwa katika maeneo mbalimbali ya jimbo. Wananchi watapata fursa ya kuuliza maswali, kutoa maoni yao na kushiriki katika kujadili masuala muhimu yanayohusu maendeleo ya kata na vijiji vyao. Ushiriki wa wananchi katika mikutano hii ni msingi m...