Kikao hicho kilijadili namna ya mahusiano ya kidiplomasia, kubadilishana uzoefu katika shughuli za kibunge, pamoja na kuimarisha sekta mbalimbali kwa manufaa ya wananchi wa Tanzania na India.
katika kikao hicho, Mhe. Kanoni alisisitiza umuhimu wa biashara wa kimataifa katika uchumi na kijamii, huku akieleza kuwa mahusiano kati ya Tanzania na India yataendelea kufungua fursa mpya za biashara, biashara, elimu na teknolojia.
Kwa upande wake, Balozi wa India alieleza utayari wa nchi yake kuchukua maoni na Tanzania katika maeneo mbalimbali ya maendeleo, akibainisha kuwa muhimu wa mabunge una mchango mkubwa katika kuimarisha uhusiano na mahusiano ya muda mrefu kati ya mataifa hayo mawili.
Kikao hicho ni sehemu ya kuimarisha diplomasia ya mabunge na mahusiano ya kirafiki kati ya Bunge la Tanzania na Bunge la India kwa manufaa ya wananchi wa pande zote mbili.
Imetolewa na
Musa Frackison Mzopola
Katibu wa jimbo Mbunge la Kalambo

