📰 HABARI MPYA
Inapakia habari...

MHE. KANONI NA WABUNGE WENZAKE WAKUTANA NA BALOZI WA INDIA KUIMARISHA MAHUSIANO KATI YA BUNGE LA TANZANIA NA BUNGE LA INDIA

MHE. KANONI NA WABUNGE WENZAKE WAKUTANA NA BALOZI WA INDIA KUIMARISHA MAHUSIANO KATI YA BUNGE LA TANZANIA NA BUNGE LA INDIA

 


Mhe. Edefonce Joackim Kanoni, Mbunge wa Jimbo la Kalambo, akiwa pamoja na wabunge wengine ambao ni wajumbe wa Chama cha Kijenga Mahusiano kati ya Bunge la Tanzania na Bunge la India, wamefanya kikao maalum na Balozi wa Jamhuri ya India nchini Tanzania kwa lengo la kuimarisha mahusiano na mahusiano kati ya nchi hizo mbili.

Kikao hicho kilijadili namna ya mahusiano ya kidiplomasia, kubadilishana uzoefu katika shughuli za kibunge, pamoja na kuimarisha sekta mbalimbali kwa manufaa ya wananchi wa Tanzania na India.

katika kikao hicho, Mhe. Kanoni alisisitiza umuhimu wa biashara wa kimataifa katika uchumi na kijamii, huku akieleza kuwa mahusiano kati ya Tanzania na India yataendelea kufungua fursa mpya za biashara, biashara, elimu na teknolojia.

Kwa upande wake, Balozi wa India alieleza utayari wa nchi yake kuchukua maoni na Tanzania katika maeneo mbalimbali ya maendeleo, akibainisha kuwa muhimu wa mabunge una mchango mkubwa katika kuimarisha uhusiano na mahusiano ya muda mrefu kati ya mataifa hayo mawili.

Kikao hicho ni sehemu ya kuimarisha diplomasia ya mabunge na mahusiano ya kirafiki kati ya Bunge la Tanzania na Bunge la India kwa manufaa ya wananchi wa pande zote mbili.

Imetolewa na

Musa Frackison Mzopola

Katibu wa jimbo Mbunge la Kalambo 


MATUKIO KWA NJIA YA PICHA

Inapakia picha...

HABARI MAARUFU

ZIARA YA MHE. KANONI KATIKA JIMBO LA KALAMBO IMEAIRISHWA; HIKI NDICHO KILICHOSABABISHA.

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo na umma kwa ujumla kuwa ziara iliyokuwa imepangwa kufanyika kuanzia tarehe 20 Julai 2026 hadi tarehe 10 Agosti 2026 imeahirishwa. Uamuzi huo umetokana na zuio la Serikali kuhusu kufanyika kwa mikutano ya hadhara katika kipindi hiki. Ofisi ya Mbunge inaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza na inaendelea kuwashukuru wananchi kwa ushirikiano na uelewa wao. Kwa taarifa zaidi na maendeleo ya shughuli za Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, tembelea: www.mbungekalambo.com Imetolewa na: Musa Frackison Mzopola Katibu wa Mbunge, Jimbo la Kalambo

HATIMAYE! ORODHA RASMI YA WANUFAIKA WA MIKOPO YA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI KWA WILAYA YA KALAMBO YATOLEWA – WANUFAIKA WOTE WATAKIWA KUHUDHURIA MAFUNZO MUHIMU

  TAARIFA KWA UMMA Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwajulisha wananchi wote wa Wilaya ya Kalambo kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekamilisha mapitio ya maombi ya mikopo yaliyowasilishwa na wananchi wa Wilaya ya Kalambo kupitia programu ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi. Kutokana na mchakato huo, Wizara imetoa rasmi orodha ya wanufaika waliokidhi vigezo na kufanikiwa kupata mikopo hiyo. Wanufaika kutoka Wilaya ya Kalambo ni kama ilivyoainishwa katika orodha rasmi ya Wizara, ambayo inajumuisha: Rahel John Mawela – Mradi wa Mbuzi Faustina Cladio Msumeno – Mradi wa Kuku wa Mayai William Isaya Moringe – Mradi wa Mbuzi Mashaka Medard Jastin – Mradi wa Mfumo wa Ubaridi Aibini Leonard John – Mradi wa Mbuzi Britney Shadi Pandisha – Mradi wa Kuku wa Nyama Sisilia Augustino Michael – Mradi wa Mbuzi Ofisi ya Mbunge inawapongeza wanufaika wote kwa kufanikiwa kupata fursa hiyo muhimu na inawatakia mafanikio katika utekelezaji wa ...

ZIARA YA MIKUTANO YA HADHARA YA MHE. EDEFONSI JOACKIM KANONI MBUNGE JIMBO LA KALAMBO YATANGAZWA

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo kuwa Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni (Mb), Mbunge wa Jimbo la Kalambo, atafanya ziara ya mikutano ya hadhara katika kata na vijiji mbalimbali vya jimbo kuanzia tarehe 20 Julai, 2026 hadi tarehe 10 Agosti, 2026, kwa mujibu wa ratiba iliyoambatanishwa.    Ziara hii inalenga kuimarisha mawasiliano kati ya Mbunge na wananchi kwa kukutana nao ana kwa ana, kusikiliza maoni, kero na changamoto zinazowakabili, pamoja na kupokea mapendekezo yatakayosaidia kuboresha huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo ya Jimbo la Kalambo. Aidha, Mhe. Mbunge atatoa mrejesho kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kueleza mipango ya maendeleo inayotarajiwa kutekelezwa katika maeneo mbalimbali ya jimbo. Wananchi watapata fursa ya kuuliza maswali, kutoa maoni yao na kushiriki katika kujadili masuala muhimu yanayohusu maendeleo ya kata na vijiji vyao. Ushiriki wa wananchi katika mikutano hii ni msingi m...