📰 HABARI MPYA
Inapakia habari...

🔥 HATIMAYE! MHE. KANONI AZINDUA KOMBE LA KANONI; AWEKA MILIONI 2 KWA MABINGWA WA LIGI YA WILAYA YA KALAMBO

🔥 HATIMAYE! MHE. KANONI AZINDUA KOMBE LA KANONI; AWEKA MILIONI 2 KWA MABINGWA WA LIGI YA WILAYA YA KALAMBO

 

TAARIFA KWA UMMA

Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni, inapenda kuwajulisha wananchi wa Wilaya ya Kalambo kuwa, miongoni mwa ahadi alizozitoa kupitia Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati wa kampeni za uchaguzi ni kuhakikisha anakuza na kuendeleza michezo pamoja na kuibua vipaji vya vijana.

Katika kutekeleza ahadi hiyo, Mhe. Mbunge amezindua Kombe la Kanoni, litakalochezwa kupitia Ligi ya Wilaya ya Kalambo, ambapo atafadhili zawadi kwa washindi kama ifuatavyo:

  • Mshindi wa Kwanza: Shilingi 1,000,000
  • Mshindi wa Pili: Shilingi 500,000
  • Mshindi wa Tatu: Shilingi 300,000
  • Mshindi wa Nne: Shilingi 200,000

Aidha, jezi na mipira pia vitatolewa kwa washindi.

Ligi itafunguliwa rasmi tarehe 05 Agosti, 2026 na itahitimishwa kwa mchezo wa fainali tarehe 11 Oktoba, 2026.

Timu zote zinazotaka kushiriki zinatakiwa kuthibitisha ushiriki wake kupitia Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Kalambo kuanzia tarehe 17 Julai, 2026 hadi tarehe 29 Julai, 2026.

Mkutano wa viongozi wa vilabu vitakavyoshiriki utafanyika tarehe 30 Julai, 2026.

Kwa maelezo zaidi kuhusu ushiriki, wasiliana na Afisa Michezo wa Wilaya kupitia namba: +255 621 650 133.

Kanda za Mashindano

  1. Kanda ya Kasanga
  2. Kanda ya Mayai
  3. Kanda ya Sopa
  4. Kanda ya Msanzi
  5. Kanda ya Mwazye
  6. Kanda ya Ulumi
  7. Kanda ya Mambwenkoswe

Washindi wa kila kanda watatinga hatua za robo fainali, nusu fainali na fainali hadi kupatikana bingwa wa Wilaya ya Kalambo, ambaye atatwaa Kombe la Kanoni pamoja na kitita cha Shilingi Milioni 1.

Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inawaomba viongozi wa kata na vijiji, Waheshimiwa Madiwani pamoja na viongozi wa timu kuhakikisha taarifa hii inawafikia wananchi na timu zote ili zipate nafasi ya kushiriki.

Pia, taasisi mbalimbali, wadau wa michezo na watu binafsi wanakaribishwa kuunga mkono jitihada hizi kwa kuchangia vifaa vya michezo na ushirikiano mwingine utakaosaidia kufanikisha ligi hii.

Imetolewa na:

Musa Frackison Mzopola
Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Kalambo


MATUKIO KWA NJIA YA PICHA

Inapakia picha...

HABARI MAARUFU

ZIARA YA MHE. KANONI KATIKA JIMBO LA KALAMBO IMEAIRISHWA; HIKI NDICHO KILICHOSABABISHA.

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo na umma kwa ujumla kuwa ziara iliyokuwa imepangwa kufanyika kuanzia tarehe 20 Julai 2026 hadi tarehe 10 Agosti 2026 imeahirishwa. Uamuzi huo umetokana na zuio la Serikali kuhusu kufanyika kwa mikutano ya hadhara katika kipindi hiki. Ofisi ya Mbunge inaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza na inaendelea kuwashukuru wananchi kwa ushirikiano na uelewa wao. Kwa taarifa zaidi na maendeleo ya shughuli za Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, tembelea: www.mbungekalambo.com Imetolewa na: Musa Frackison Mzopola Katibu wa Mbunge, Jimbo la Kalambo

HATIMAYE! ORODHA RASMI YA WANUFAIKA WA MIKOPO YA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI KWA WILAYA YA KALAMBO YATOLEWA – WANUFAIKA WOTE WATAKIWA KUHUDHURIA MAFUNZO MUHIMU

  TAARIFA KWA UMMA Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwajulisha wananchi wote wa Wilaya ya Kalambo kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekamilisha mapitio ya maombi ya mikopo yaliyowasilishwa na wananchi wa Wilaya ya Kalambo kupitia programu ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi. Kutokana na mchakato huo, Wizara imetoa rasmi orodha ya wanufaika waliokidhi vigezo na kufanikiwa kupata mikopo hiyo. Wanufaika kutoka Wilaya ya Kalambo ni kama ilivyoainishwa katika orodha rasmi ya Wizara, ambayo inajumuisha: Rahel John Mawela – Mradi wa Mbuzi Faustina Cladio Msumeno – Mradi wa Kuku wa Mayai William Isaya Moringe – Mradi wa Mbuzi Mashaka Medard Jastin – Mradi wa Mfumo wa Ubaridi Aibini Leonard John – Mradi wa Mbuzi Britney Shadi Pandisha – Mradi wa Kuku wa Nyama Sisilia Augustino Michael – Mradi wa Mbuzi Ofisi ya Mbunge inawapongeza wanufaika wote kwa kufanikiwa kupata fursa hiyo muhimu na inawatakia mafanikio katika utekelezaji wa ...

ZIARA YA MIKUTANO YA HADHARA YA MHE. EDEFONSI JOACKIM KANONI MBUNGE JIMBO LA KALAMBO YATANGAZWA

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo kuwa Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni (Mb), Mbunge wa Jimbo la Kalambo, atafanya ziara ya mikutano ya hadhara katika kata na vijiji mbalimbali vya jimbo kuanzia tarehe 20 Julai, 2026 hadi tarehe 10 Agosti, 2026, kwa mujibu wa ratiba iliyoambatanishwa.    Ziara hii inalenga kuimarisha mawasiliano kati ya Mbunge na wananchi kwa kukutana nao ana kwa ana, kusikiliza maoni, kero na changamoto zinazowakabili, pamoja na kupokea mapendekezo yatakayosaidia kuboresha huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo ya Jimbo la Kalambo. Aidha, Mhe. Mbunge atatoa mrejesho kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kueleza mipango ya maendeleo inayotarajiwa kutekelezwa katika maeneo mbalimbali ya jimbo. Wananchi watapata fursa ya kuuliza maswali, kutoa maoni yao na kushiriki katika kujadili masuala muhimu yanayohusu maendeleo ya kata na vijiji vyao. Ushiriki wa wananchi katika mikutano hii ni msingi m...