📰 HABARI MPYA
Inapakia habari...

🔥 HATIMAYE! MHE. KANONI AZINDUA KOMBE LA KANONI; AWEKA MILIONI 2 KWA MABINGWA WA LIGI YA WILAYA YA KALAMBO

🔥 HATIMAYE! MHE. KANONI AZINDUA KOMBE LA KANONI; AWEKA MILIONI 2 KWA MABINGWA WA LIGI YA WILAYA YA KALAMBO

 

TAARIFA KWA UMMA

Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni, inapenda kuwajulisha wananchi wa Wilaya ya Kalambo kuwa, miongoni mwa ahadi alizozitoa kupitia Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati wa kampeni za uchaguzi ni kuhakikisha anakuza na kuendeleza michezo pamoja na kuibua vipaji vya vijana.

Katika kutekeleza ahadi hiyo, Mhe. Mbunge amezindua Kombe la Kanoni, litakalochezwa kupitia Ligi ya Wilaya ya Kalambo, ambapo atafadhili zawadi kwa washindi kama ifuatavyo:

  • Mshindi wa Kwanza: Shilingi 1,000,000
  • Mshindi wa Pili: Shilingi 500,000
  • Mshindi wa Tatu: Shilingi 300,000
  • Mshindi wa Nne: Shilingi 200,000

Aidha, jezi na mipira pia vitatolewa kwa washindi.

Ligi itafunguliwa rasmi tarehe 05 Agosti, 2026 na itahitimishwa kwa mchezo wa fainali tarehe 11 Oktoba, 2026.

Timu zote zinazotaka kushiriki zinatakiwa kuthibitisha ushiriki wake kupitia Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Kalambo kuanzia tarehe 17 Julai, 2026 hadi tarehe 29 Julai, 2026.

Mkutano wa viongozi wa vilabu vitakavyoshiriki utafanyika tarehe 30 Julai, 2026.

Kwa maelezo zaidi kuhusu ushiriki, wasiliana na Afisa Michezo wa Wilaya kupitia namba: +255 621 650 133.

Kanda za Mashindano

  1. Kanda ya Kasanga
  2. Kanda ya Mayai
  3. Kanda ya Sopa
  4. Kanda ya Msanzi
  5. Kanda ya Mwazye
  6. Kanda ya Ulumi
  7. Kanda ya Mambwenkoswe

Washindi wa kila kanda watatinga hatua za robo fainali, nusu fainali na fainali hadi kupatikana bingwa wa Wilaya ya Kalambo, ambaye atatwaa Kombe la Kanoni pamoja na kitita cha Shilingi Milioni 1.

Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inawaomba viongozi wa kata na vijiji, Waheshimiwa Madiwani pamoja na viongozi wa timu kuhakikisha taarifa hii inawafikia wananchi na timu zote ili zipate nafasi ya kushiriki.

Pia, taasisi mbalimbali, wadau wa michezo na watu binafsi wanakaribishwa kuunga mkono jitihada hizi kwa kuchangia vifaa vya michezo na ushirikiano mwingine utakaosaidia kufanikisha ligi hii.

Imetolewa na:

Musa Frackison Mzopola
Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Kalambo


Umemaliza kusoma habari hii? Tupe maoni, mtazamo au swali lako hapa chini.

Comments

MATUKIO KWA NJIA YA PICHA

Inapakia picha...

HABARI MAARUFU

FURSA ZA MIKOPO YA VIJANA SASA HADHARANI OMBA SASA UJIKWAMUE KIUCHUMI

  Katika kutekeleza ahadi ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya kutoa shilingi bilioni 200 kwa vijana ndani ya siku 100 baada ya kuingia madarakani, Wizara ya Mifugo na Uvuvi inautangazia umma kuanza kwa Awamu ya Pili ya utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu kwa vijana. Malengo ya mikopo hiyo ni kuwawezesha vijana kupata mitaji ya kuanzisha na kuendeleza biashara ndogo, biashara za kati na kampuni changa ili kujijengea kipato katika Sekta za Mifugo na Uvuvi. Mikopo hiyo itatolewa kwa njia ya vifaa na pembejeo za uzalishaji, ikiwemo ufugaji wa samaki kwa vizimba, ufugaji wa kuku (chotara, mayai na nyama), mbuzi, kondoo na nguruwe, pamoja na boti za kuhudumia vizimba, boti za uvuvi, zana za uvuvi, mifumo ya ubari (cold chain) katika mazao ya uvuvi, mifumo ya kulazisha vifaranga vya samaki, mifumo na vifaa vya uchakataji wa mazao ya uvuvi ikijumuisha makausho ya dagaa na mwani (dryers). Vigezo na maelekezo kwa waombaji ni kama ifuatavyo: i. Baru...

NAFASI 200 ZA AJIRA ZA MAFUNDI ZATANGAZWA KWA KAZI NCHINI SAUDI ARABIA

  Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, kwa kushirikiana na Atilis Investment Limited , inawataarifu Watanzania wenye sifa stahiki kuhusu nafasi 200 za ajira za mafundi katika sekta ya ujenzi , zilizotolewa na kampuni ya Shade Corporation Limited ya nchini Saudi Arabia. KADA ZINAZOHITAJIKA Nafasi hizo zinahusisha mafundi wa kada mbalimbali, wakiwemo: Mafundi Uashi Mafundi Useremala Wasuka Nondo SIFA ZA MWOMBAJI Mwombaji anatakiwa kuwa na: Elimu ya astashahada kutoka chuo cha ufundi kinachotambuliwa na Serikali; Uzoefu wa kazi wa miaka miwili (2) au zaidi katika sekta ya ufundi; Uwezo na uzoefu katika kada husika, ikiwemo Uashi, Useremala au Usuka Nondo; Umri kati ya miaka 21 hadi 40 ; Waombaji wa nafasi hizi wanatakiwa kuwa wanaume . MASHARTI NA MAFANO YA AJIRA Waombaji watakaofaulu mchakato wa ajira watapata fursa ya kufanya kazi nchini Saudi Arabia kwa masharti yaliyowekwa na mwajiri. Miongoni mwa mafao na masharti ya ajira ni: Mshahara wa Riyal 1...

MHE. MBUNGE KANONI ASHIRIKI MAZISHI YA WAATHIRIKA WA AJALI KAZILA, ATOA WITO WA UPENDO, UMOJA NA MSHIKAMANO

  KALAMBO: Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , ameshiriki mazishi ya wananchi wawili waliofariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea katika Kijiji cha Kazila, Kata ya Mwazye, Wilaya ya Kalambo, huku akitoa pole na faraja kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki pamoja na wananchi wote walioguswa na msiba huo. Ajali hiyo ilitokea tarehe 05 Agosti 2026 , wakati gari aina ya Fuso lililokuwa limebeba watu waliokuwa wakielekea kwenye shughuli ya harusi kutoka Kijiji cha Msoma, Kata ya Mwazye, Wilaya ya Kalambo , lilipofika katika Kijiji cha Kazila kwa ajili ya shughuli ya kufunga ndoa. Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa, gari hilo lilikuwa limembeba bwana harusi, Hosea Gilbert Watua , pamoja na watu wengine waliokuwa wakisafiri naye kutoka Kijiji cha Msoma kuelekea Kijiji cha Kazila, ambako alikuwa akienda kufunga ndoa na bibi harusi, Mehili Sauli Visent , mkazi wa Kijiji cha Kazila, Kata ya Mwazye. AJALI YATOKEA KABLA YA KUFIKA KWENYE DARAJA Taarifa zinaeleza ...