TAARIFA KWA UMMA
Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni, inapenda kuwajulisha wananchi wa Wilaya ya Kalambo kuwa, miongoni mwa ahadi alizozitoa kupitia Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati wa kampeni za uchaguzi ni kuhakikisha anakuza na kuendeleza michezo pamoja na kuibua vipaji vya vijana.
Katika kutekeleza ahadi hiyo, Mhe. Mbunge amezindua Kombe la Kanoni, litakalochezwa kupitia Ligi ya Wilaya ya Kalambo, ambapo atafadhili zawadi kwa washindi kama ifuatavyo:
- Mshindi wa Kwanza: Shilingi 1,000,000
- Mshindi wa Pili: Shilingi 500,000
- Mshindi wa Tatu: Shilingi 300,000
- Mshindi wa Nne: Shilingi 200,000
Aidha, jezi na mipira pia vitatolewa kwa washindi.
Ligi itafunguliwa rasmi tarehe 05 Agosti, 2026 na itahitimishwa kwa mchezo wa fainali tarehe 11 Oktoba, 2026.
Timu zote zinazotaka kushiriki zinatakiwa kuthibitisha ushiriki wake kupitia Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Kalambo kuanzia tarehe 17 Julai, 2026 hadi tarehe 29 Julai, 2026.
Mkutano wa viongozi wa vilabu vitakavyoshiriki utafanyika tarehe 30 Julai, 2026.
Kwa maelezo zaidi kuhusu ushiriki, wasiliana na Afisa Michezo wa Wilaya kupitia namba: +255 621 650 133.
Kanda za Mashindano
- Kanda ya Kasanga
- Kanda ya Mayai
- Kanda ya Sopa
- Kanda ya Msanzi
- Kanda ya Mwazye
- Kanda ya Ulumi
- Kanda ya Mambwenkoswe
Washindi wa kila kanda watatinga hatua za robo fainali, nusu fainali na fainali hadi kupatikana bingwa wa Wilaya ya Kalambo, ambaye atatwaa Kombe la Kanoni pamoja na kitita cha Shilingi Milioni 1.
Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inawaomba viongozi wa kata na vijiji, Waheshimiwa Madiwani pamoja na viongozi wa timu kuhakikisha taarifa hii inawafikia wananchi na timu zote ili zipate nafasi ya kushiriki.
Pia, taasisi mbalimbali, wadau wa michezo na watu binafsi wanakaribishwa kuunga mkono jitihada hizi kwa kuchangia vifaa vya michezo na ushirikiano mwingine utakaosaidia kufanikisha ligi hii.
Imetolewa na:
Musa Frackison Mzopola
Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Kalambo

