📰 HABARI MPYA
Inapakia habari...

🔥 HATIMAYE UJENZI WA STENDI YA KISASA KALAMBO WAANZA RASMI – HATUA MPYA YA MAENDELEO KWA WANANCHI!

 🔥 HATIMAYE UJENZI WA STENDI YA KISASA KALAMBO WAANZA RASMI – HATUA MPYA YA MAENDELEO KWA WANANCHI!

 

TAARIFA KWA UMMA
KUTOKA OFISI YA MBUNGE WA JIMBO LA KALAMBO, MHE. EDEFONSI JOACKIM KANONI

Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni, inapenda kuwajulisha wananchi wote wa Jimbo la Kalambo kuwa ujenzi wa Stendi ya Kisasa, ambao unatekelezwa kwa fedha milioni 300 zilizotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tayari umeanza rasmi.

Hii ni hatua muhimu katika safari ya maendeleo ya Jimbo letu, ikiwa ni matokeo ya ushirikiano kati ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Wizara husika, viongozi wa Serikali, watendaji mbalimbali pamoja na juhudi za Mbunge wetu katika kuwasilisha na kufuatilia mahitaji ya wananchi wa Kalambo.

Kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Kalambo, tunatoa shukrani za dhati kwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mawaziri, viongozi na watendaji wote wa Serikali kwa kuendelea kusikiliza na kutekeleza mahitaji ya wananchi. Ujenzi huu ni ushahidi kuwa pale ambapo viongozi na wananchi wanashirikiana kwa dhati, maendeleo hupatikana.

Aidha, tunaendelea kuiomba Serikali kuendelea kuzipatia fedha miradi mingine ya maendeleo ambayo imewasilishwa na Mheshimiwa Mbunge kwa niaba ya wananchi pamoja na mahitaji yaliyowasilishwa na idara mbalimbali za Wilaya ya Kalambo. Tuna imani kuwa kwa ushirikiano uliopo, miradi mingi zaidi itaendelea kutekelezwa kwa manufaa ya wananchi.

Ofisi ya Mbunge inatoa wito kwa wananchi wote kuendelea kudumisha umoja, upendo, mshikamano na ushirikiano. Maendeleo si jukumu la Serikali pekee wala la Mbunge pekee, bali ni wajibu wa kila mwananchi. Tunaposhirikiana, kuheshimiana na kushiriki kikamilifu katika mipango ya maendeleo, tunaijenga Kalambo yenye ustawi na fursa kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Vilevile, tunawakumbusha watumishi wote wa umma kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa weledi, uadilifu na uzalendo. Wananchi wanahitaji huduma bora, za haki na zinazotolewa kwa wakati. Kila mtumishi anapaswa kutanguliza maslahi ya Taifa na wananchi mbele ya maslahi binafsi, kwani maendeleo ya nchi yetu yanategemea uwajibikaji wa kila mmoja katika nafasi yake.

Tukumbuke kuwa maendeleo ya kweli yanajengwa kwa umoja, ushirikiano, uwajibikaji na ushirikishwaji wa wananchi katika kila hatua ya maendeleo. Tukiendelea kushikamana, Kalambo itaendelea kuwa mfano wa maendeleo yanayowagusa wananchi wote.

Kazi na Utu, Tunasonga Mbele.

Imetolewa na:

Musa Frackison Mzopola
Katibu wa Mbunge
Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo


MATUKIO KWA NJIA YA PICHA

Inapakia picha...

HABARI MAARUFU

ZIARA YA MHE. KANONI KATIKA JIMBO LA KALAMBO IMEAIRISHWA; HIKI NDICHO KILICHOSABABISHA.

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo na umma kwa ujumla kuwa ziara iliyokuwa imepangwa kufanyika kuanzia tarehe 20 Julai 2026 hadi tarehe 10 Agosti 2026 imeahirishwa. Uamuzi huo umetokana na zuio la Serikali kuhusu kufanyika kwa mikutano ya hadhara katika kipindi hiki. Ofisi ya Mbunge inaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza na inaendelea kuwashukuru wananchi kwa ushirikiano na uelewa wao. Kwa taarifa zaidi na maendeleo ya shughuli za Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, tembelea: www.mbungekalambo.com Imetolewa na: Musa Frackison Mzopola Katibu wa Mbunge, Jimbo la Kalambo

HATIMAYE! ORODHA RASMI YA WANUFAIKA WA MIKOPO YA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI KWA WILAYA YA KALAMBO YATOLEWA – WANUFAIKA WOTE WATAKIWA KUHUDHURIA MAFUNZO MUHIMU

  TAARIFA KWA UMMA Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwajulisha wananchi wote wa Wilaya ya Kalambo kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekamilisha mapitio ya maombi ya mikopo yaliyowasilishwa na wananchi wa Wilaya ya Kalambo kupitia programu ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi. Kutokana na mchakato huo, Wizara imetoa rasmi orodha ya wanufaika waliokidhi vigezo na kufanikiwa kupata mikopo hiyo. Wanufaika kutoka Wilaya ya Kalambo ni kama ilivyoainishwa katika orodha rasmi ya Wizara, ambayo inajumuisha: Rahel John Mawela – Mradi wa Mbuzi Faustina Cladio Msumeno – Mradi wa Kuku wa Mayai William Isaya Moringe – Mradi wa Mbuzi Mashaka Medard Jastin – Mradi wa Mfumo wa Ubaridi Aibini Leonard John – Mradi wa Mbuzi Britney Shadi Pandisha – Mradi wa Kuku wa Nyama Sisilia Augustino Michael – Mradi wa Mbuzi Ofisi ya Mbunge inawapongeza wanufaika wote kwa kufanikiwa kupata fursa hiyo muhimu na inawatakia mafanikio katika utekelezaji wa ...

ZIARA YA MIKUTANO YA HADHARA YA MHE. EDEFONSI JOACKIM KANONI MBUNGE JIMBO LA KALAMBO YATANGAZWA

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo kuwa Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni (Mb), Mbunge wa Jimbo la Kalambo, atafanya ziara ya mikutano ya hadhara katika kata na vijiji mbalimbali vya jimbo kuanzia tarehe 20 Julai, 2026 hadi tarehe 10 Agosti, 2026, kwa mujibu wa ratiba iliyoambatanishwa.    Ziara hii inalenga kuimarisha mawasiliano kati ya Mbunge na wananchi kwa kukutana nao ana kwa ana, kusikiliza maoni, kero na changamoto zinazowakabili, pamoja na kupokea mapendekezo yatakayosaidia kuboresha huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo ya Jimbo la Kalambo. Aidha, Mhe. Mbunge atatoa mrejesho kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kueleza mipango ya maendeleo inayotarajiwa kutekelezwa katika maeneo mbalimbali ya jimbo. Wananchi watapata fursa ya kuuliza maswali, kutoa maoni yao na kushiriki katika kujadili masuala muhimu yanayohusu maendeleo ya kata na vijiji vyao. Ushiriki wa wananchi katika mikutano hii ni msingi m...