📰 HABARI MPYA
Inapakia habari...

🔥 HATIMAYE UJENZI WA STENDI YA KISASA KALAMBO WAANZA RASMI – HATUA MPYA YA MAENDELEO KWA WANANCHI!

 🔥 HATIMAYE UJENZI WA STENDI YA KISASA KALAMBO WAANZA RASMI – HATUA MPYA YA MAENDELEO KWA WANANCHI!

 

TAARIFA KWA UMMA
KUTOKA OFISI YA MBUNGE WA JIMBO LA KALAMBO, MHE. EDEFONSI JOACKIM KANONI

Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni, inapenda kuwajulisha wananchi wote wa Jimbo la Kalambo kuwa ujenzi wa Stendi ya Kisasa, ambao unatekelezwa kwa fedha milioni 300 zilizotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tayari umeanza rasmi.

Hii ni hatua muhimu katika safari ya maendeleo ya Jimbo letu, ikiwa ni matokeo ya ushirikiano kati ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Wizara husika, viongozi wa Serikali, watendaji mbalimbali pamoja na juhudi za Mbunge wetu katika kuwasilisha na kufuatilia mahitaji ya wananchi wa Kalambo.

Kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Kalambo, tunatoa shukrani za dhati kwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mawaziri, viongozi na watendaji wote wa Serikali kwa kuendelea kusikiliza na kutekeleza mahitaji ya wananchi. Ujenzi huu ni ushahidi kuwa pale ambapo viongozi na wananchi wanashirikiana kwa dhati, maendeleo hupatikana.

Aidha, tunaendelea kuiomba Serikali kuendelea kuzipatia fedha miradi mingine ya maendeleo ambayo imewasilishwa na Mheshimiwa Mbunge kwa niaba ya wananchi pamoja na mahitaji yaliyowasilishwa na idara mbalimbali za Wilaya ya Kalambo. Tuna imani kuwa kwa ushirikiano uliopo, miradi mingi zaidi itaendelea kutekelezwa kwa manufaa ya wananchi.

Ofisi ya Mbunge inatoa wito kwa wananchi wote kuendelea kudumisha umoja, upendo, mshikamano na ushirikiano. Maendeleo si jukumu la Serikali pekee wala la Mbunge pekee, bali ni wajibu wa kila mwananchi. Tunaposhirikiana, kuheshimiana na kushiriki kikamilifu katika mipango ya maendeleo, tunaijenga Kalambo yenye ustawi na fursa kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Vilevile, tunawakumbusha watumishi wote wa umma kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa weledi, uadilifu na uzalendo. Wananchi wanahitaji huduma bora, za haki na zinazotolewa kwa wakati. Kila mtumishi anapaswa kutanguliza maslahi ya Taifa na wananchi mbele ya maslahi binafsi, kwani maendeleo ya nchi yetu yanategemea uwajibikaji wa kila mmoja katika nafasi yake.

Tukumbuke kuwa maendeleo ya kweli yanajengwa kwa umoja, ushirikiano, uwajibikaji na ushirikishwaji wa wananchi katika kila hatua ya maendeleo. Tukiendelea kushikamana, Kalambo itaendelea kuwa mfano wa maendeleo yanayowagusa wananchi wote.

Kazi na Utu, Tunasonga Mbele.

Imetolewa na:

Musa Frackison Mzopola
Katibu wa Mbunge
Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo


Umemaliza kusoma habari hii? Tupe maoni, mtazamo au swali lako hapa chini.

Comments

MATUKIO KWA NJIA YA PICHA

Inapakia picha...

HABARI MAARUFU

FURSA ZA MIKOPO YA VIJANA SASA HADHARANI OMBA SASA UJIKWAMUE KIUCHUMI

  Katika kutekeleza ahadi ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya kutoa shilingi bilioni 200 kwa vijana ndani ya siku 100 baada ya kuingia madarakani, Wizara ya Mifugo na Uvuvi inautangazia umma kuanza kwa Awamu ya Pili ya utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu kwa vijana. Malengo ya mikopo hiyo ni kuwawezesha vijana kupata mitaji ya kuanzisha na kuendeleza biashara ndogo, biashara za kati na kampuni changa ili kujijengea kipato katika Sekta za Mifugo na Uvuvi. Mikopo hiyo itatolewa kwa njia ya vifaa na pembejeo za uzalishaji, ikiwemo ufugaji wa samaki kwa vizimba, ufugaji wa kuku (chotara, mayai na nyama), mbuzi, kondoo na nguruwe, pamoja na boti za kuhudumia vizimba, boti za uvuvi, zana za uvuvi, mifumo ya ubari (cold chain) katika mazao ya uvuvi, mifumo ya kulazisha vifaranga vya samaki, mifumo na vifaa vya uchakataji wa mazao ya uvuvi ikijumuisha makausho ya dagaa na mwani (dryers). Vigezo na maelekezo kwa waombaji ni kama ifuatavyo: i. Baru...

NAFASI 200 ZA AJIRA ZA MAFUNDI ZATANGAZWA KWA KAZI NCHINI SAUDI ARABIA

  Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, kwa kushirikiana na Atilis Investment Limited , inawataarifu Watanzania wenye sifa stahiki kuhusu nafasi 200 za ajira za mafundi katika sekta ya ujenzi , zilizotolewa na kampuni ya Shade Corporation Limited ya nchini Saudi Arabia. KADA ZINAZOHITAJIKA Nafasi hizo zinahusisha mafundi wa kada mbalimbali, wakiwemo: Mafundi Uashi Mafundi Useremala Wasuka Nondo SIFA ZA MWOMBAJI Mwombaji anatakiwa kuwa na: Elimu ya astashahada kutoka chuo cha ufundi kinachotambuliwa na Serikali; Uzoefu wa kazi wa miaka miwili (2) au zaidi katika sekta ya ufundi; Uwezo na uzoefu katika kada husika, ikiwemo Uashi, Useremala au Usuka Nondo; Umri kati ya miaka 21 hadi 40 ; Waombaji wa nafasi hizi wanatakiwa kuwa wanaume . MASHARTI NA MAFANO YA AJIRA Waombaji watakaofaulu mchakato wa ajira watapata fursa ya kufanya kazi nchini Saudi Arabia kwa masharti yaliyowekwa na mwajiri. Miongoni mwa mafao na masharti ya ajira ni: Mshahara wa Riyal 1...

MHE. MBUNGE KANONI ASHIRIKI MAZISHI YA WAATHIRIKA WA AJALI KAZILA, ATOA WITO WA UPENDO, UMOJA NA MSHIKAMANO

  KALAMBO: Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , ameshiriki mazishi ya wananchi wawili waliofariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea katika Kijiji cha Kazila, Kata ya Mwazye, Wilaya ya Kalambo, huku akitoa pole na faraja kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki pamoja na wananchi wote walioguswa na msiba huo. Ajali hiyo ilitokea tarehe 05 Agosti 2026 , wakati gari aina ya Fuso lililokuwa limebeba watu waliokuwa wakielekea kwenye shughuli ya harusi kutoka Kijiji cha Msoma, Kata ya Mwazye, Wilaya ya Kalambo , lilipofika katika Kijiji cha Kazila kwa ajili ya shughuli ya kufunga ndoa. Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa, gari hilo lilikuwa limembeba bwana harusi, Hosea Gilbert Watua , pamoja na watu wengine waliokuwa wakisafiri naye kutoka Kijiji cha Msoma kuelekea Kijiji cha Kazila, ambako alikuwa akienda kufunga ndoa na bibi harusi, Mehili Sauli Visent , mkazi wa Kijiji cha Kazila, Kata ya Mwazye. AJALI YATOKEA KABLA YA KUFIKA KWENYE DARAJA Taarifa zinaeleza ...