Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo na Watanzania kwa ujumla kuwa Mheshimiwa Edifonsi Joackim Kanoni, Mbunge wa Jimbo la Kalambo, ameandaa bonanza kubwa la michezo litakalojulikana kwa jina la KANONI SUPER BONANZA, litakalofanyika kuanzia tarehe 06 Julai, 2026 hadi tarehe 07 Julai, 2026.
Bonanza hilo limeandaliwa kwa lengo la kuendeleza na kuhamasisha michezo, kukuza vipaji vya vijana, kuimarisha afya za wananchi, pamoja na kuendeleza umoja, mshikamano na ushirikiano miongoni mwa wananchi wa Jimbo la Kalambo.
Timu zitakazoshiriki katika bonanza hilo ni:
Matai FC
Chapakazi FC
Motochini VS
Nyota Njema FC
Uzinduzi rasmi wa KANONI SUPER BONANZA utafanyika tarehe 06 Julai, 2026, uwanja wa Kateka kata ya Matai wilaya Kalambo ambapo Mheshimiwa Edifonsi Joackim Kanoni, Mbunge wa Jimbo la Kalambo, atakuwa Mgeni Rasmi.
Akizungumzia maandalizi ya bonanza hilo, Mheshimiwa Kanoni amesema kuwa michezo ni nyenzo muhimu ya kuimarisha afya, kuibua vipaji, kujenga urafiki na kuimarisha mshikamano wa wananchi. Ameeleza kuwa Ofisi yake itaendelea kuwekeza katika maendeleo ya michezo kama sehemu ya kuwatumikia wananchi na kuwajengea vijana mazingira bora ya kukuza vipaji vyao.
Aidha, Ofisi ya Mbunge inawakaribisha wananchi wote wa Jimbo la Kalambo kujitokeza kwa wingi kushuhudia na kushiriki katika bonanza hilo ili kuendelea kuimarisha umoja, upendo na mshikamano ambao ni msingi wa maendeleo ya Jimbo letu.
Kazi na Utu, Tunasonga Mbele.
Imetolewa na:
MUSA FRACKISON MZOPOPA
Katibu wa Mbunge Jimbo la Kalambo

