📰 HABARI MPYA
Inapakia habari...

KANONI SUPER BONANZA KUANZA JULAI 6–7, 2026 KALAMBO

KANONI SUPER BONANZA KUANZA JULAI 6–7, 2026 KALAMBO

 

Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo na Watanzania kwa ujumla kuwa Mheshimiwa Edifonsi Joackim Kanoni, Mbunge wa Jimbo la Kalambo, ameandaa bonanza kubwa la michezo litakalojulikana kwa jina la KANONI SUPER BONANZA, litakalofanyika kuanzia tarehe 06 Julai, 2026 hadi tarehe 07 Julai, 2026.

Bonanza hilo limeandaliwa kwa lengo la kuendeleza na kuhamasisha michezo, kukuza vipaji vya vijana, kuimarisha afya za wananchi, pamoja na kuendeleza umoja, mshikamano na ushirikiano miongoni mwa wananchi wa Jimbo la Kalambo.

Timu zitakazoshiriki katika bonanza hilo ni:

  • Matai FC

  • Chapakazi FC

  • Motochini VS

  • Nyota Njema FC

Uzinduzi rasmi wa KANONI SUPER BONANZA utafanyika tarehe 06 Julai, 2026, uwanja wa Kateka kata ya Matai wilaya Kalambo ambapo Mheshimiwa Edifonsi Joackim Kanoni, Mbunge wa Jimbo la Kalambo, atakuwa Mgeni Rasmi.

Akizungumzia maandalizi ya bonanza hilo, Mheshimiwa Kanoni amesema kuwa michezo ni nyenzo muhimu ya kuimarisha afya, kuibua vipaji, kujenga urafiki na kuimarisha mshikamano wa wananchi. Ameeleza kuwa Ofisi yake itaendelea kuwekeza katika maendeleo ya michezo kama sehemu ya kuwatumikia wananchi na kuwajengea vijana mazingira bora ya kukuza vipaji vyao.

Aidha, Ofisi ya Mbunge inawakaribisha wananchi wote wa Jimbo la Kalambo kujitokeza kwa wingi kushuhudia na kushiriki katika bonanza hilo ili kuendelea kuimarisha umoja, upendo na mshikamano ambao ni msingi wa maendeleo ya Jimbo letu.

Kazi na Utu, Tunasonga Mbele.

Imetolewa na:

MUSA FRACKISON MZOPOPA
Katibu wa Mbunge Jimbo la Kalambo

MATUKIO KWA NJIA YA PICHA

Inapakia picha...

HABARI MAARUFU

ZIARA YA MHE. KANONI KATIKA JIMBO LA KALAMBO IMEAIRISHWA; HIKI NDICHO KILICHOSABABISHA.

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo na umma kwa ujumla kuwa ziara iliyokuwa imepangwa kufanyika kuanzia tarehe 20 Julai 2026 hadi tarehe 10 Agosti 2026 imeahirishwa. Uamuzi huo umetokana na zuio la Serikali kuhusu kufanyika kwa mikutano ya hadhara katika kipindi hiki. Ofisi ya Mbunge inaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza na inaendelea kuwashukuru wananchi kwa ushirikiano na uelewa wao. Kwa taarifa zaidi na maendeleo ya shughuli za Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, tembelea: www.mbungekalambo.com Imetolewa na: Musa Frackison Mzopola Katibu wa Mbunge, Jimbo la Kalambo

HATIMAYE! ORODHA RASMI YA WANUFAIKA WA MIKOPO YA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI KWA WILAYA YA KALAMBO YATOLEWA – WANUFAIKA WOTE WATAKIWA KUHUDHURIA MAFUNZO MUHIMU

  TAARIFA KWA UMMA Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwajulisha wananchi wote wa Wilaya ya Kalambo kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekamilisha mapitio ya maombi ya mikopo yaliyowasilishwa na wananchi wa Wilaya ya Kalambo kupitia programu ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi. Kutokana na mchakato huo, Wizara imetoa rasmi orodha ya wanufaika waliokidhi vigezo na kufanikiwa kupata mikopo hiyo. Wanufaika kutoka Wilaya ya Kalambo ni kama ilivyoainishwa katika orodha rasmi ya Wizara, ambayo inajumuisha: Rahel John Mawela – Mradi wa Mbuzi Faustina Cladio Msumeno – Mradi wa Kuku wa Mayai William Isaya Moringe – Mradi wa Mbuzi Mashaka Medard Jastin – Mradi wa Mfumo wa Ubaridi Aibini Leonard John – Mradi wa Mbuzi Britney Shadi Pandisha – Mradi wa Kuku wa Nyama Sisilia Augustino Michael – Mradi wa Mbuzi Ofisi ya Mbunge inawapongeza wanufaika wote kwa kufanikiwa kupata fursa hiyo muhimu na inawatakia mafanikio katika utekelezaji wa ...

ZIARA YA MIKUTANO YA HADHARA YA MHE. EDEFONSI JOACKIM KANONI MBUNGE JIMBO LA KALAMBO YATANGAZWA

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo kuwa Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni (Mb), Mbunge wa Jimbo la Kalambo, atafanya ziara ya mikutano ya hadhara katika kata na vijiji mbalimbali vya jimbo kuanzia tarehe 20 Julai, 2026 hadi tarehe 10 Agosti, 2026, kwa mujibu wa ratiba iliyoambatanishwa.    Ziara hii inalenga kuimarisha mawasiliano kati ya Mbunge na wananchi kwa kukutana nao ana kwa ana, kusikiliza maoni, kero na changamoto zinazowakabili, pamoja na kupokea mapendekezo yatakayosaidia kuboresha huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo ya Jimbo la Kalambo. Aidha, Mhe. Mbunge atatoa mrejesho kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kueleza mipango ya maendeleo inayotarajiwa kutekelezwa katika maeneo mbalimbali ya jimbo. Wananchi watapata fursa ya kuuliza maswali, kutoa maoni yao na kushiriki katika kujadili masuala muhimu yanayohusu maendeleo ya kata na vijiji vyao. Ushiriki wa wananchi katika mikutano hii ni msingi m...