📰 HABARI MPYA
Inapakia habari...

KIKUNDI CHA TUINUANE MADIBILA KUNUFAIKA NA MKOPO WA SHILINGI MILIONI 100 KWA AJILI YA UNUNUZI WA TRAKTA

KIKUNDI CHA TUINUANE MADIBILA KUNUFAIKA NA MKOPO WA SHILINGI MILIONI 100 KWA AJILI YA UNUNUZI WA TRAKTA

KALAMBO: Kikundi cha Tuinuane kilichopo katika Kijiji cha Madibila, Jimbo la Kalambo, kimefanikiwa kunufaika na mkopo wa Shilingi Milioni 100 kwa ajili ya ununuzi wa trekta aina ya New Holland, kupitia mpango wa mikopo wa Serikali unaotekelezwa kupitia Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana.

Kikundi hicho ni miongoni mwa wanufaika wa mpango wa mikopo wenye thamani ya Shilingi Bilioni 200, unaotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Upatikanaji wa mkopo huo umewezekana kwa juhudi za Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni, ambaye amesaidia kufuatilia na kuwezesha upatikanaji wa fursa hiyo kupitia Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana.

Trekta aina ya New Holland, ambayo ni miongoni mwa matrekta bora na imara, inatarajiwa kuongeza tija katika shughuli za kilimo, kupunguza changamoto za upatikanaji wa huduma za kilimo na kuchochea maendeleo ya kiuchumi kwa wanakikundi pamoja na wananchi wa Kalambo kwa ujumla.

Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo imetoa shukrani za dhati kwa Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kujali, kuthamini na kuunga mkono juhudi za maendeleo ya wananchi wa Kalambo.

Aidha, Ofisi ya Mbunge imetoa shukrani maalum kwa Mhe. Joel Arthur Nanauka, Waziri wa Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, pamoja na Mawaziri na watendaji wote wa Serikali, kwa juhudi na ushirikiano wao katika kuhakikisha wananchi wanapata fursa za kiuchumi na mikopo yenye tija.

Pamoja na mafanikio hayo, Ofisi ya Mbunge inaendelea kuiomba Serikali kuendelea kutoa na kuongeza fursa za mikopo kwa wananchi wa Kalambo, hususan mikopo ya vizimba katika Ziwa Tanganyika pamoja na mikopo ya ufugaji, ili kuwawezesha wananchi wengi zaidi kushiriki katika shughuli za uzalishaji na kujikwamua kiuchumi.

Ofisi ya Mbunge inatoa wito kwa wananchi wote wa Kalambo kuendelea kudumisha upendo, umoja na mshikamano, kwa kuwa umoja na mshikamano wa wananchi ni msingi muhimu katika kuendeleza na kuijenga Kalambo yenye maendeleo endelevu.

Imetolewa na:
MUSA FRACKISON MZOPOLA
KATIBU WA MBUNGE
JIMBO LA KALAMBO


MATUKIO KWA NJIA YA PICHA

Inapakia picha...

HABARI MAARUFU

ZIARA YA MHE. KANONI KATIKA JIMBO LA KALAMBO IMEAIRISHWA; HIKI NDICHO KILICHOSABABISHA.

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo na umma kwa ujumla kuwa ziara iliyokuwa imepangwa kufanyika kuanzia tarehe 20 Julai 2026 hadi tarehe 10 Agosti 2026 imeahirishwa. Uamuzi huo umetokana na zuio la Serikali kuhusu kufanyika kwa mikutano ya hadhara katika kipindi hiki. Ofisi ya Mbunge inaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza na inaendelea kuwashukuru wananchi kwa ushirikiano na uelewa wao. Kwa taarifa zaidi na maendeleo ya shughuli za Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, tembelea: www.mbungekalambo.com Imetolewa na: Musa Frackison Mzopola Katibu wa Mbunge, Jimbo la Kalambo

HATIMAYE! ORODHA RASMI YA WANUFAIKA WA MIKOPO YA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI KWA WILAYA YA KALAMBO YATOLEWA – WANUFAIKA WOTE WATAKIWA KUHUDHURIA MAFUNZO MUHIMU

  TAARIFA KWA UMMA Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwajulisha wananchi wote wa Wilaya ya Kalambo kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekamilisha mapitio ya maombi ya mikopo yaliyowasilishwa na wananchi wa Wilaya ya Kalambo kupitia programu ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi. Kutokana na mchakato huo, Wizara imetoa rasmi orodha ya wanufaika waliokidhi vigezo na kufanikiwa kupata mikopo hiyo. Wanufaika kutoka Wilaya ya Kalambo ni kama ilivyoainishwa katika orodha rasmi ya Wizara, ambayo inajumuisha: Rahel John Mawela – Mradi wa Mbuzi Faustina Cladio Msumeno – Mradi wa Kuku wa Mayai William Isaya Moringe – Mradi wa Mbuzi Mashaka Medard Jastin – Mradi wa Mfumo wa Ubaridi Aibini Leonard John – Mradi wa Mbuzi Britney Shadi Pandisha – Mradi wa Kuku wa Nyama Sisilia Augustino Michael – Mradi wa Mbuzi Ofisi ya Mbunge inawapongeza wanufaika wote kwa kufanikiwa kupata fursa hiyo muhimu na inawatakia mafanikio katika utekelezaji wa ...

ZIARA YA MIKUTANO YA HADHARA YA MHE. EDEFONSI JOACKIM KANONI MBUNGE JIMBO LA KALAMBO YATANGAZWA

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo kuwa Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni (Mb), Mbunge wa Jimbo la Kalambo, atafanya ziara ya mikutano ya hadhara katika kata na vijiji mbalimbali vya jimbo kuanzia tarehe 20 Julai, 2026 hadi tarehe 10 Agosti, 2026, kwa mujibu wa ratiba iliyoambatanishwa.    Ziara hii inalenga kuimarisha mawasiliano kati ya Mbunge na wananchi kwa kukutana nao ana kwa ana, kusikiliza maoni, kero na changamoto zinazowakabili, pamoja na kupokea mapendekezo yatakayosaidia kuboresha huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo ya Jimbo la Kalambo. Aidha, Mhe. Mbunge atatoa mrejesho kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kueleza mipango ya maendeleo inayotarajiwa kutekelezwa katika maeneo mbalimbali ya jimbo. Wananchi watapata fursa ya kuuliza maswali, kutoa maoni yao na kushiriki katika kujadili masuala muhimu yanayohusu maendeleo ya kata na vijiji vyao. Ushiriki wa wananchi katika mikutano hii ni msingi m...