Msaada huo umetolewa kufuatia ombi lililotolewa na vijana wa kijiji hicho wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika mwezi Aprili, ambapo walimweleza Mbunge changamoto ya ukosefu wa vifaa vya michezo. Utekelezaji huu unaonesha dhamira ya kweli ya Mhe. Kanoni ya kusikiliza wananchi na kutekeleza ahadi alizozitoa kwa wakati.
Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo kwa niaba ya Mbunge, Ndugu Musa Frackison Mzopola alisema kuwa Mhe. Kanoni anatambua mchango mkubwa wa michezo katika kujenga afya, kuimarisha umoja wa vijana, kukuza vipaji na kuondoa vitendo vinavyoweza kuhatarisha amani na maendeleo ya jamii.
Aidha, amewatangazia wananchi wa Kalambo kuwa, kama Mhe Mbunge alivyoahidi kuanzia mwezi Julai ofisi ya Mbunge imeanza utaratibu wa kutoa vifaa vya michezo kwa vikundi na timu mbalimbali zilizoomba msaada huo katika maeneo tofauti ya Jimbo la Kalambo. Alisisitiza kuwa waombaji wote watapatiwa huduma hiyo hatua kwa hatua, hivyo aliwaomba waendelee kuwa na subira wakati taratibu za ugawaji zikiendelea.
Vilevile, alieleza kuwa Mhe. Mbunge anatarajia kuanza tena ziara za mikutano ya hadhara katika vijiji mbalimbali vya Jimbo la Kalambo. Katika ziara hizo, ataendelea kusikiliza kero za wananchi, kufuatilia utekelezaji wa ahadi alizotoa na kukabidhi misaada mbalimbali katika maeneo yaliyoiomba.
Kwa upande wake, aliwahimiza vijana kutumia vipaji vyao kama njia ya kujiletea maendeleo na kujiongezea kipato, huku akiwataka kujiepusha na vitendo vya uhalifu, matumizi ya dawa za kulevya na mambo yote yanayoweza kuvuruga amani, utulivu na mshikamano wa Taifa letu.
Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inaendelea kuwahimiza wananchi wote kushirikiana na Serikali katika kuleta maendeleo ya Jimbo letu. Ushirikiano, umoja, upendo na mshikamano ndiyo msingi wa kufanikisha miradi ya maendeleo na kujenga Kalambo yenye ustawi kwa kizazi cha sasa na kijacho.
Mhe. Edifonsi Joackim Kanoni anaendelea kuwathibitishia wananchi kuwa yuko bega kwa bega nao katika kutatua changamoto zao na kuhakikisha ahadi zote zinazotekelezeka zinafanyiwa kazi kwa vitendo kwa manufaa ya wananchi wote.
KAZI NA UTU TUNASONGAMBELE
Imetolewa na:
Musa Frackison Mzopola
Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Kalambo

