📰 HABARI MPYA
Inapakia habari...

MHE KANONI AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA KALAMBO YATOA MIKOPO YA ASILIMIA 10 YENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 50 KWA VIKUNDI

MHE KANONI AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA KALAMBO YATOA MIKOPO YA ASILIMIA 10 YENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 50 KWA VIKUNDI

 




Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edifonsi Joackim Kanoni, imepongeza Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo kwa kufanikisha utoaji wa mikopo ya asilimia 10 yenye thamani ya Shilingi milioni 50 kwa vikundi mbalimbali mwezi Mei 2026. Hatua hiyo inaonesha dhamira ya Serikali ya kuwawezesha wananchi kiuchumi, hususan vijana, wanawake na makundi maalum, kupitia fursa za mikopo kwa ajili ya kukuza shughuli za uzalishaji mali, kuongeza ajira na kuinua uchumi wa wananchi wa Wilaya ya Kalambo.

Vikundi vilivyonufaika na mikopo hiyo ni:

  1. Kikundi cha Wanawake Ilolesha – Kijiji cha Myunga, Kata ya Mkali – Shilingi 3,000,000.
  2. Kikundi cha Vijana Umoja ni Nguvu – Kijiji cha Mikonko, Kata ya Matai – Shilingi 10,000,000.
  3. Kikundi cha Walemavu – Kijiji cha Santamaria, Kata ya Lyowa – Shilingi 5,000,000.
  4. Kikundi cha Wanawake Ushindi – Kijiji cha Mao, Kata ya Mbuluma – Shilingi 8,000,000.
  5. Kikundi cha Ukuuwa Fashion – Kijiji cha Kasanga, Kata ya Kasanga – Shilingi 3,000,000.
  6. Kikundi cha Vijana Twaweza – Kijiji cha Mtula, Kata ya Mnamba – Shilingi 7,000,000.
  7. Kikundi cha Vijana Urafiki – Kijiji cha Kambo, Kata ya Kilesha – Shilingi 5,000,000.
  8. Agro-farm Group – Kijiji cha Kifone, Kata ya Kilesha – Shilingi 5,000,000.
  9. Kikundi cha Vijana cha Mito ya Baraka – Kijiji cha Kisala, Kata ya Samazi – Shilingi 4,000,000.

Jumla ya Shilingi milioni 50 zimetolewa kwa vikundi hivyo kwa lengo la kuongeza mitaji, kukuza shughuli za uzalishaji mali, kuongeza ajira na kuinua uchumi wa wananchi wa Wilaya ya Kalambo.

Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inawahimiza vijana wengine kujitokeza kuunda vikundi vinavyokidhi vigezo ili waweze kunufaika na fursa za mikopo inayotolewa na Serikali. Vijana wanapaswa kuelekeza nguvu zao katika kufanya kazi kwa bidii, ubunifu na uzalendo, huku wakiepuka kujiingiza katika makundi yenye mienendo inayoweza kuvuruga amani, umoja na utulivu wa nchi yetu.

Aidha, Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inatoa wito kwa wananchi wote wa Kalambo kuendelea kudumisha umoja, mshikamano na ushirikiano katika kuharakisha maendeleo ya wilaya. Maendeleo ya Kalambo yanategemea ushirikiano wa wananchi wote pamoja na matumizi sahihi ya fursa zinazotolewa na Serikali kwa manufaa ya jamii.

KAZI NA UTU TUNASONGA MBELE

Imetolewa na:

Musa Frackison Mzopola
Katibu wa Mbunge, Jimbo la Kalambo


MATUKIO KWA NJIA YA PICHA

Inapakia picha...

HABARI MAARUFU

ZIARA YA MHE. KANONI KATIKA JIMBO LA KALAMBO IMEAIRISHWA; HIKI NDICHO KILICHOSABABISHA.

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo na umma kwa ujumla kuwa ziara iliyokuwa imepangwa kufanyika kuanzia tarehe 20 Julai 2026 hadi tarehe 10 Agosti 2026 imeahirishwa. Uamuzi huo umetokana na zuio la Serikali kuhusu kufanyika kwa mikutano ya hadhara katika kipindi hiki. Ofisi ya Mbunge inaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza na inaendelea kuwashukuru wananchi kwa ushirikiano na uelewa wao. Kwa taarifa zaidi na maendeleo ya shughuli za Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, tembelea: www.mbungekalambo.com Imetolewa na: Musa Frackison Mzopola Katibu wa Mbunge, Jimbo la Kalambo

HATIMAYE! ORODHA RASMI YA WANUFAIKA WA MIKOPO YA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI KWA WILAYA YA KALAMBO YATOLEWA – WANUFAIKA WOTE WATAKIWA KUHUDHURIA MAFUNZO MUHIMU

  TAARIFA KWA UMMA Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwajulisha wananchi wote wa Wilaya ya Kalambo kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekamilisha mapitio ya maombi ya mikopo yaliyowasilishwa na wananchi wa Wilaya ya Kalambo kupitia programu ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi. Kutokana na mchakato huo, Wizara imetoa rasmi orodha ya wanufaika waliokidhi vigezo na kufanikiwa kupata mikopo hiyo. Wanufaika kutoka Wilaya ya Kalambo ni kama ilivyoainishwa katika orodha rasmi ya Wizara, ambayo inajumuisha: Rahel John Mawela – Mradi wa Mbuzi Faustina Cladio Msumeno – Mradi wa Kuku wa Mayai William Isaya Moringe – Mradi wa Mbuzi Mashaka Medard Jastin – Mradi wa Mfumo wa Ubaridi Aibini Leonard John – Mradi wa Mbuzi Britney Shadi Pandisha – Mradi wa Kuku wa Nyama Sisilia Augustino Michael – Mradi wa Mbuzi Ofisi ya Mbunge inawapongeza wanufaika wote kwa kufanikiwa kupata fursa hiyo muhimu na inawatakia mafanikio katika utekelezaji wa ...

ZIARA YA MIKUTANO YA HADHARA YA MHE. EDEFONSI JOACKIM KANONI MBUNGE JIMBO LA KALAMBO YATANGAZWA

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo kuwa Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni (Mb), Mbunge wa Jimbo la Kalambo, atafanya ziara ya mikutano ya hadhara katika kata na vijiji mbalimbali vya jimbo kuanzia tarehe 20 Julai, 2026 hadi tarehe 10 Agosti, 2026, kwa mujibu wa ratiba iliyoambatanishwa.    Ziara hii inalenga kuimarisha mawasiliano kati ya Mbunge na wananchi kwa kukutana nao ana kwa ana, kusikiliza maoni, kero na changamoto zinazowakabili, pamoja na kupokea mapendekezo yatakayosaidia kuboresha huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo ya Jimbo la Kalambo. Aidha, Mhe. Mbunge atatoa mrejesho kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kueleza mipango ya maendeleo inayotarajiwa kutekelezwa katika maeneo mbalimbali ya jimbo. Wananchi watapata fursa ya kuuliza maswali, kutoa maoni yao na kushiriki katika kujadili masuala muhimu yanayohusu maendeleo ya kata na vijiji vyao. Ushiriki wa wananchi katika mikutano hii ni msingi m...