Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edifonsi Joackim Kanoni, imepongeza Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo kwa kufanikisha utoaji wa mikopo ya asilimia 10 yenye thamani ya Shilingi milioni 50 kwa vikundi mbalimbali mwezi Mei 2026. Hatua hiyo inaonesha dhamira ya Serikali ya kuwawezesha wananchi kiuchumi, hususan vijana, wanawake na makundi maalum, kupitia fursa za mikopo kwa ajili ya kukuza shughuli za uzalishaji mali, kuongeza ajira na kuinua uchumi wa wananchi wa Wilaya ya Kalambo.
Vikundi vilivyonufaika na mikopo hiyo ni:
- Kikundi cha Wanawake Ilolesha – Kijiji cha Myunga, Kata ya Mkali – Shilingi 3,000,000.
- Kikundi cha Vijana Umoja ni Nguvu – Kijiji cha Mikonko, Kata ya Matai – Shilingi 10,000,000.
- Kikundi cha Walemavu – Kijiji cha Santamaria, Kata ya Lyowa – Shilingi 5,000,000.
- Kikundi cha Wanawake Ushindi – Kijiji cha Mao, Kata ya Mbuluma – Shilingi 8,000,000.
- Kikundi cha Ukuuwa Fashion – Kijiji cha Kasanga, Kata ya Kasanga – Shilingi 3,000,000.
- Kikundi cha Vijana Twaweza – Kijiji cha Mtula, Kata ya Mnamba – Shilingi 7,000,000.
- Kikundi cha Vijana Urafiki – Kijiji cha Kambo, Kata ya Kilesha – Shilingi 5,000,000.
- Agro-farm Group – Kijiji cha Kifone, Kata ya Kilesha – Shilingi 5,000,000.
- Kikundi cha Vijana cha Mito ya Baraka – Kijiji cha Kisala, Kata ya Samazi – Shilingi 4,000,000.
Jumla ya Shilingi milioni 50 zimetolewa kwa vikundi hivyo kwa lengo la kuongeza mitaji, kukuza shughuli za uzalishaji mali, kuongeza ajira na kuinua uchumi wa wananchi wa Wilaya ya Kalambo.
Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inawahimiza vijana wengine kujitokeza kuunda vikundi vinavyokidhi vigezo ili waweze kunufaika na fursa za mikopo inayotolewa na Serikali. Vijana wanapaswa kuelekeza nguvu zao katika kufanya kazi kwa bidii, ubunifu na uzalendo, huku wakiepuka kujiingiza katika makundi yenye mienendo inayoweza kuvuruga amani, umoja na utulivu wa nchi yetu.
Aidha, Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inatoa wito kwa wananchi wote wa Kalambo kuendelea kudumisha umoja, mshikamano na ushirikiano katika kuharakisha maendeleo ya wilaya. Maendeleo ya Kalambo yanategemea ushirikiano wa wananchi wote pamoja na matumizi sahihi ya fursa zinazotolewa na Serikali kwa manufaa ya jamii.
KAZI NA UTU TUNASONGA MBELE
Imetolewa na:
Musa Frackison Mzopola
Katibu wa Mbunge, Jimbo la Kalambo

