📰 HABARI MPYA
Inapakia habari...

SERIKALI YAMJIBU MHE. KANONI KWA VITENDO; YATOA FEDHA ZA UJENZI WA MIRADI YA ELIMU KALAMBO

SERIKALI YAMJIBU MHE. KANONI KWA VITENDO; YATOA FEDHA ZA UJENZI WA MIRADI YA ELIMU KALAMBO

Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni, inapenda kutoa shukrani za dhati kwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Mawaziri, viongozi na watendaji wote wa Serikali kwa kuendelea kusikiliza na kutekeleza kwa vitendo maombi yaliyowasilishwa kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wa Jimbo la Kalambo.

Ofisi ya Mbunge imepokea kwa furaha taarifa ya kutolewa kwa fedha za utekelezaji wa miradi mbalimbali ya elimu, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa madarasa matano (5) na matundu kumi (10) ya vyoo katika Shule ya Msingi Msoma, Kata ya Mwazye, ujenzi wa madarasa matano (5) na matundu kumi (10) ya vyoo katika Shule ya Msingi Mzungwa, Kata ya Mambwenkoswe, pamoja na fedha za ujenzi wa Kituo cha Walimu katika Kijiji cha Kalembe, Kata ya Mambwenkoswe 

Hatua hii ni uthibitisho kuwa Serikali inaendelea kuwajali na kuwathamini wananchi wa Kalambo kwa kutekeleza miradi yenye lengo la kuboresha huduma za elimu na kuinua ustawi wa jamii.

Pamoja na mafanikio hayo, Ofisi ya Mbunge inaendelea kuiomba Serikali kuidhinisha fedha zaidi kwa ajili ya kukamilisha miradi mingine ya maendeleo ambayo imewasilishwa, ili wananchi wa Kalambo waendelee kunufaika na huduma bora katika sekta mbalimbali.

Aidha, Mhe. Kanoni anatoa wito kwa wananchi wote wa Jimbo la Kalambo kuendelea kudumisha umoja, upendo, mshikamano na ushirikiano, kwani maendeleo ya kweli yanapatikana pale wananchi wanaposhirikiana na kuunga mkono juhudi za Serikali katika kutekeleza miradi ya maendeleo.

Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inaendelea kuwahakikishia wananchi kuwa itaendelea kusimamia na kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa ahadi na miradi yote ya maendeleo kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

 

Imetolewa na


Musa Frackison Mzopola

Katibu wa Mbunge Jimbo la Kalambo

MATUKIO KWA NJIA YA PICHA

Inapakia picha...

HABARI MAARUFU

ZIARA YA MHE. KANONI KATIKA JIMBO LA KALAMBO IMEAIRISHWA; HIKI NDICHO KILICHOSABABISHA.

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo na umma kwa ujumla kuwa ziara iliyokuwa imepangwa kufanyika kuanzia tarehe 20 Julai 2026 hadi tarehe 10 Agosti 2026 imeahirishwa. Uamuzi huo umetokana na zuio la Serikali kuhusu kufanyika kwa mikutano ya hadhara katika kipindi hiki. Ofisi ya Mbunge inaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza na inaendelea kuwashukuru wananchi kwa ushirikiano na uelewa wao. Kwa taarifa zaidi na maendeleo ya shughuli za Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, tembelea: www.mbungekalambo.com Imetolewa na: Musa Frackison Mzopola Katibu wa Mbunge, Jimbo la Kalambo

HATIMAYE! ORODHA RASMI YA WANUFAIKA WA MIKOPO YA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI KWA WILAYA YA KALAMBO YATOLEWA – WANUFAIKA WOTE WATAKIWA KUHUDHURIA MAFUNZO MUHIMU

  TAARIFA KWA UMMA Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwajulisha wananchi wote wa Wilaya ya Kalambo kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekamilisha mapitio ya maombi ya mikopo yaliyowasilishwa na wananchi wa Wilaya ya Kalambo kupitia programu ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi. Kutokana na mchakato huo, Wizara imetoa rasmi orodha ya wanufaika waliokidhi vigezo na kufanikiwa kupata mikopo hiyo. Wanufaika kutoka Wilaya ya Kalambo ni kama ilivyoainishwa katika orodha rasmi ya Wizara, ambayo inajumuisha: Rahel John Mawela – Mradi wa Mbuzi Faustina Cladio Msumeno – Mradi wa Kuku wa Mayai William Isaya Moringe – Mradi wa Mbuzi Mashaka Medard Jastin – Mradi wa Mfumo wa Ubaridi Aibini Leonard John – Mradi wa Mbuzi Britney Shadi Pandisha – Mradi wa Kuku wa Nyama Sisilia Augustino Michael – Mradi wa Mbuzi Ofisi ya Mbunge inawapongeza wanufaika wote kwa kufanikiwa kupata fursa hiyo muhimu na inawatakia mafanikio katika utekelezaji wa ...

ZIARA YA MIKUTANO YA HADHARA YA MHE. EDEFONSI JOACKIM KANONI MBUNGE JIMBO LA KALAMBO YATANGAZWA

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo kuwa Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni (Mb), Mbunge wa Jimbo la Kalambo, atafanya ziara ya mikutano ya hadhara katika kata na vijiji mbalimbali vya jimbo kuanzia tarehe 20 Julai, 2026 hadi tarehe 10 Agosti, 2026, kwa mujibu wa ratiba iliyoambatanishwa.    Ziara hii inalenga kuimarisha mawasiliano kati ya Mbunge na wananchi kwa kukutana nao ana kwa ana, kusikiliza maoni, kero na changamoto zinazowakabili, pamoja na kupokea mapendekezo yatakayosaidia kuboresha huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo ya Jimbo la Kalambo. Aidha, Mhe. Mbunge atatoa mrejesho kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kueleza mipango ya maendeleo inayotarajiwa kutekelezwa katika maeneo mbalimbali ya jimbo. Wananchi watapata fursa ya kuuliza maswali, kutoa maoni yao na kushiriki katika kujadili masuala muhimu yanayohusu maendeleo ya kata na vijiji vyao. Ushiriki wa wananchi katika mikutano hii ni msingi m...