Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inapenda kuwajulisha wananchi wote wa Wilaya ya Kalambo kuhusu fursa ya kupata mikopo ya kilimo kutoka Benki ya CRDB, Tawi la Sumbawanga, kwa wakulima mmoja mmoja.
Masharti ya kupata mkopo
Mwombaji anatakiwa kutimiza vigezo vifuatavyo:
Awe na shamba la kuanzia hekari 10 au zaidi.
Awe na nyumba au dhamana inayokubalika na benki kwa ajili ya kudhamini mkopo.
Atimize taratibu na masharti mengine ya Benki ya CRDB wakati wa maombi.
Kiasi cha mkopo
Mkopo hutolewa kulingana na ukubwa wa shamba:
Kwa kila hekari moja, mkulima anaweza kupata kati ya Shilingi 850,000 hadi Shilingi 1,000,000.
Mfano, mkulima mwenye hekari 10 anaweza kupata mkopo wa kati ya Shilingi Milioni 8.5 hadi Milioni 10, kulingana na tathmini ya benki.
Riba na ulipaji
Riba ya mkopo ni asilimia 17.
Marejesho ya mkopo hufanyika baada ya mkulima kuvuna na kuuza mazao yake, NFRA, kulingana na utaratibu wa benki.
Bima ya mkopo
Mkopo huu unaambatana na bima ya kilimo. Endapo kutatokea majanga ya asili kama:
Ukame au mvua kutonyesha,
Kimbunga,
Au maafa mengine yanayoharibu mazao kwa mujibu wa masharti ya bima,
bima inaweza kugharamia deni la mkopo kwa kadiri ya masharti yake. Hata hivyo, endapo hasara itasababishwa na uzembe wa mkopaji au kutofuata kanuni za kilimo, mkopaji atawajibika mwenyewe kulipa mkopo.
Mahali pa kuchukua fomu
Wananchi wote wenye sifa wanakaribishwa kuchukua fomu za maombi ya mkopo katika Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo.
Mwisho wa kuchukua fomu ni tarehe 30/07/2026. Hivyo, wote wanaohitaji mkopo wanashauriwa kufika ofisini mapema kabla ya tarehe ya mwisho.
Ukipata taarifa hii, tafadhali mjulishe na mwenzako ili wote wanufaike na fursa hii.
Imetolewa na:
Musa Frackison Mzopola
Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Kalambo

