📰 HABARI MPYA
Inapakia habari...

TAARIFA YA FURSA YA MIKOPO YA KILIMO KUTOKA BENKI YA CRDB

TAARIFA YA FURSA YA MIKOPO YA KILIMO KUTOKA BENKI YA CRDB

 


Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inapenda kuwajulisha wananchi wote wa Wilaya ya Kalambo kuhusu fursa ya kupata mikopo ya kilimo kutoka Benki ya CRDB, Tawi la Sumbawanga, kwa wakulima mmoja mmoja.

Masharti ya kupata mkopo

Mwombaji anatakiwa kutimiza vigezo vifuatavyo:

Awe na shamba la kuanzia hekari 10 au zaidi.

Awe na nyumba au dhamana inayokubalika na benki kwa ajili ya kudhamini mkopo.

Atimize taratibu na masharti mengine ya Benki ya CRDB wakati wa maombi.

Kiasi cha mkopo

Mkopo hutolewa kulingana na ukubwa wa shamba:

Kwa kila hekari moja, mkulima anaweza kupata kati ya Shilingi 850,000 hadi Shilingi 1,000,000.

Mfano, mkulima mwenye hekari 10 anaweza kupata mkopo wa kati ya Shilingi Milioni 8.5 hadi Milioni 10, kulingana na tathmini ya benki.

Riba na ulipaji

Riba ya mkopo ni asilimia 17.

Marejesho ya mkopo hufanyika baada ya mkulima kuvuna na kuuza mazao yake,  NFRA, kulingana na utaratibu wa benki.

Bima ya mkopo

Mkopo huu unaambatana na bima ya kilimo. Endapo kutatokea majanga ya asili kama:

Ukame au mvua kutonyesha,

Kimbunga,

Au maafa mengine yanayoharibu mazao kwa mujibu wa masharti ya bima,

bima inaweza kugharamia deni la mkopo kwa kadiri ya masharti yake. Hata hivyo, endapo hasara itasababishwa na uzembe wa mkopaji au kutofuata kanuni za kilimo, mkopaji atawajibika mwenyewe kulipa mkopo.

Mahali pa kuchukua fomu

Wananchi wote wenye sifa wanakaribishwa kuchukua fomu za maombi ya mkopo katika Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo.

Mwisho wa kuchukua fomu ni tarehe 30/07/2026. Hivyo, wote wanaohitaji mkopo wanashauriwa kufika ofisini mapema kabla ya tarehe ya mwisho.

Ukipata taarifa hii, tafadhali mjulishe na mwenzako ili wote wanufaike na fursa hii.

Imetolewa na:

Musa Frackison Mzopola
Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Kalambo

MATUKIO KWA NJIA YA PICHA

Inapakia picha...

HABARI MAARUFU

ZIARA YA MHE. KANONI KATIKA JIMBO LA KALAMBO IMEAIRISHWA; HIKI NDICHO KILICHOSABABISHA.

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo na umma kwa ujumla kuwa ziara iliyokuwa imepangwa kufanyika kuanzia tarehe 20 Julai 2026 hadi tarehe 10 Agosti 2026 imeahirishwa. Uamuzi huo umetokana na zuio la Serikali kuhusu kufanyika kwa mikutano ya hadhara katika kipindi hiki. Ofisi ya Mbunge inaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza na inaendelea kuwashukuru wananchi kwa ushirikiano na uelewa wao. Kwa taarifa zaidi na maendeleo ya shughuli za Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, tembelea: www.mbungekalambo.com Imetolewa na: Musa Frackison Mzopola Katibu wa Mbunge, Jimbo la Kalambo

HATIMAYE! ORODHA RASMI YA WANUFAIKA WA MIKOPO YA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI KWA WILAYA YA KALAMBO YATOLEWA – WANUFAIKA WOTE WATAKIWA KUHUDHURIA MAFUNZO MUHIMU

  TAARIFA KWA UMMA Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwajulisha wananchi wote wa Wilaya ya Kalambo kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekamilisha mapitio ya maombi ya mikopo yaliyowasilishwa na wananchi wa Wilaya ya Kalambo kupitia programu ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi. Kutokana na mchakato huo, Wizara imetoa rasmi orodha ya wanufaika waliokidhi vigezo na kufanikiwa kupata mikopo hiyo. Wanufaika kutoka Wilaya ya Kalambo ni kama ilivyoainishwa katika orodha rasmi ya Wizara, ambayo inajumuisha: Rahel John Mawela – Mradi wa Mbuzi Faustina Cladio Msumeno – Mradi wa Kuku wa Mayai William Isaya Moringe – Mradi wa Mbuzi Mashaka Medard Jastin – Mradi wa Mfumo wa Ubaridi Aibini Leonard John – Mradi wa Mbuzi Britney Shadi Pandisha – Mradi wa Kuku wa Nyama Sisilia Augustino Michael – Mradi wa Mbuzi Ofisi ya Mbunge inawapongeza wanufaika wote kwa kufanikiwa kupata fursa hiyo muhimu na inawatakia mafanikio katika utekelezaji wa ...

ZIARA YA MIKUTANO YA HADHARA YA MHE. EDEFONSI JOACKIM KANONI MBUNGE JIMBO LA KALAMBO YATANGAZWA

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo kuwa Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni (Mb), Mbunge wa Jimbo la Kalambo, atafanya ziara ya mikutano ya hadhara katika kata na vijiji mbalimbali vya jimbo kuanzia tarehe 20 Julai, 2026 hadi tarehe 10 Agosti, 2026, kwa mujibu wa ratiba iliyoambatanishwa.    Ziara hii inalenga kuimarisha mawasiliano kati ya Mbunge na wananchi kwa kukutana nao ana kwa ana, kusikiliza maoni, kero na changamoto zinazowakabili, pamoja na kupokea mapendekezo yatakayosaidia kuboresha huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo ya Jimbo la Kalambo. Aidha, Mhe. Mbunge atatoa mrejesho kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kueleza mipango ya maendeleo inayotarajiwa kutekelezwa katika maeneo mbalimbali ya jimbo. Wananchi watapata fursa ya kuuliza maswali, kutoa maoni yao na kushiriki katika kujadili masuala muhimu yanayohusu maendeleo ya kata na vijiji vyao. Ushiriki wa wananchi katika mikutano hii ni msingi m...