📰 HABARI MPYA
Inapakia habari...

TAARIFA YA FURSA YA MIKOPO YA KILIMO KUTOKA BENKI YA CRDB

TAARIFA YA FURSA YA MIKOPO YA KILIMO KUTOKA BENKI YA CRDB

 


Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inapenda kuwajulisha wananchi wote wa Wilaya ya Kalambo kuhusu fursa ya kupata mikopo ya kilimo kutoka Benki ya CRDB, Tawi la Sumbawanga, kwa wakulima mmoja mmoja.

Masharti ya kupata mkopo

Mwombaji anatakiwa kutimiza vigezo vifuatavyo:

Awe na shamba la kuanzia hekari 10 au zaidi.

Awe na nyumba au dhamana inayokubalika na benki kwa ajili ya kudhamini mkopo.

Atimize taratibu na masharti mengine ya Benki ya CRDB wakati wa maombi.

Kiasi cha mkopo

Mkopo hutolewa kulingana na ukubwa wa shamba:

Kwa kila hekari moja, mkulima anaweza kupata kati ya Shilingi 850,000 hadi Shilingi 1,000,000.

Mfano, mkulima mwenye hekari 10 anaweza kupata mkopo wa kati ya Shilingi Milioni 8.5 hadi Milioni 10, kulingana na tathmini ya benki.

Riba na ulipaji

Riba ya mkopo ni asilimia 17.

Marejesho ya mkopo hufanyika baada ya mkulima kuvuna na kuuza mazao yake,  NFRA, kulingana na utaratibu wa benki.

Bima ya mkopo

Mkopo huu unaambatana na bima ya kilimo. Endapo kutatokea majanga ya asili kama:

Ukame au mvua kutonyesha,

Kimbunga,

Au maafa mengine yanayoharibu mazao kwa mujibu wa masharti ya bima,

bima inaweza kugharamia deni la mkopo kwa kadiri ya masharti yake. Hata hivyo, endapo hasara itasababishwa na uzembe wa mkopaji au kutofuata kanuni za kilimo, mkopaji atawajibika mwenyewe kulipa mkopo.

Mahali pa kuchukua fomu

Wananchi wote wenye sifa wanakaribishwa kuchukua fomu za maombi ya mkopo katika Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo.

Mwisho wa kuchukua fomu ni tarehe 30/07/2026. Hivyo, wote wanaohitaji mkopo wanashauriwa kufika ofisini mapema kabla ya tarehe ya mwisho.

Ukipata taarifa hii, tafadhali mjulishe na mwenzako ili wote wanufaike na fursa hii.

Imetolewa na:

Musa Frackison Mzopola
Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Kalambo

Umemaliza kusoma habari hii? Tupe maoni, mtazamo au swali lako hapa chini.

Comments

MATUKIO KWA NJIA YA PICHA

Inapakia picha...

HABARI MAARUFU

FURSA ZA MIKOPO YA VIJANA SASA HADHARANI OMBA SASA UJIKWAMUE KIUCHUMI

  Katika kutekeleza ahadi ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya kutoa shilingi bilioni 200 kwa vijana ndani ya siku 100 baada ya kuingia madarakani, Wizara ya Mifugo na Uvuvi inautangazia umma kuanza kwa Awamu ya Pili ya utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu kwa vijana. Malengo ya mikopo hiyo ni kuwawezesha vijana kupata mitaji ya kuanzisha na kuendeleza biashara ndogo, biashara za kati na kampuni changa ili kujijengea kipato katika Sekta za Mifugo na Uvuvi. Mikopo hiyo itatolewa kwa njia ya vifaa na pembejeo za uzalishaji, ikiwemo ufugaji wa samaki kwa vizimba, ufugaji wa kuku (chotara, mayai na nyama), mbuzi, kondoo na nguruwe, pamoja na boti za kuhudumia vizimba, boti za uvuvi, zana za uvuvi, mifumo ya ubari (cold chain) katika mazao ya uvuvi, mifumo ya kulazisha vifaranga vya samaki, mifumo na vifaa vya uchakataji wa mazao ya uvuvi ikijumuisha makausho ya dagaa na mwani (dryers). Vigezo na maelekezo kwa waombaji ni kama ifuatavyo: i. Baru...

NAFASI 200 ZA AJIRA ZA MAFUNDI ZATANGAZWA KWA KAZI NCHINI SAUDI ARABIA

  Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, kwa kushirikiana na Atilis Investment Limited , inawataarifu Watanzania wenye sifa stahiki kuhusu nafasi 200 za ajira za mafundi katika sekta ya ujenzi , zilizotolewa na kampuni ya Shade Corporation Limited ya nchini Saudi Arabia. KADA ZINAZOHITAJIKA Nafasi hizo zinahusisha mafundi wa kada mbalimbali, wakiwemo: Mafundi Uashi Mafundi Useremala Wasuka Nondo SIFA ZA MWOMBAJI Mwombaji anatakiwa kuwa na: Elimu ya astashahada kutoka chuo cha ufundi kinachotambuliwa na Serikali; Uzoefu wa kazi wa miaka miwili (2) au zaidi katika sekta ya ufundi; Uwezo na uzoefu katika kada husika, ikiwemo Uashi, Useremala au Usuka Nondo; Umri kati ya miaka 21 hadi 40 ; Waombaji wa nafasi hizi wanatakiwa kuwa wanaume . MASHARTI NA MAFANO YA AJIRA Waombaji watakaofaulu mchakato wa ajira watapata fursa ya kufanya kazi nchini Saudi Arabia kwa masharti yaliyowekwa na mwajiri. Miongoni mwa mafao na masharti ya ajira ni: Mshahara wa Riyal 1...

MHE. MBUNGE KANONI ASHIRIKI MAZISHI YA WAATHIRIKA WA AJALI KAZILA, ATOA WITO WA UPENDO, UMOJA NA MSHIKAMANO

  KALAMBO: Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , ameshiriki mazishi ya wananchi wawili waliofariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea katika Kijiji cha Kazila, Kata ya Mwazye, Wilaya ya Kalambo, huku akitoa pole na faraja kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki pamoja na wananchi wote walioguswa na msiba huo. Ajali hiyo ilitokea tarehe 05 Agosti 2026 , wakati gari aina ya Fuso lililokuwa limebeba watu waliokuwa wakielekea kwenye shughuli ya harusi kutoka Kijiji cha Msoma, Kata ya Mwazye, Wilaya ya Kalambo , lilipofika katika Kijiji cha Kazila kwa ajili ya shughuli ya kufunga ndoa. Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa, gari hilo lilikuwa limembeba bwana harusi, Hosea Gilbert Watua , pamoja na watu wengine waliokuwa wakisafiri naye kutoka Kijiji cha Msoma kuelekea Kijiji cha Kazila, ambako alikuwa akienda kufunga ndoa na bibi harusi, Mehili Sauli Visent , mkazi wa Kijiji cha Kazila, Kata ya Mwazye. AJALI YATOKEA KABLA YA KUFIKA KWENYE DARAJA Taarifa zinaeleza ...