Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo kuwa Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni (Mb), Mbunge wa Jimbo la Kalambo, atafanya ziara ya mikutano ya hadhara katika kata na vijiji mbalimbali vya jimbo kuanzia tarehe 20 Julai, 2026 hadi tarehe 10 Agosti, 2026, kwa mujibu wa ratiba iliyoambatanishwa.
Ziara hii inalenga kuimarisha mawasiliano kati ya Mbunge na wananchi kwa kukutana nao ana kwa ana, kusikiliza maoni, kero na changamoto zinazowakabili, pamoja na kupokea mapendekezo yatakayosaidia kuboresha huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo ya Jimbo la Kalambo. Aidha, Mhe. Mbunge atatoa mrejesho kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kueleza mipango ya maendeleo inayotarajiwa kutekelezwa katika maeneo mbalimbali ya jimbo.
Wananchi watapata fursa ya kuuliza maswali, kutoa maoni yao na kushiriki katika kujadili masuala muhimu yanayohusu maendeleo ya kata na vijiji vyao. Ushiriki wa wananchi katika mikutano hii ni msingi muhimu wa uongozi shirikishi na maendeleo endelevu.
Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inawaomba wananchi wote kujitokeza kwa wingi katika mikutano hiyo kulingana na ratiba ifuatayo ili waweze kumsikia Mbunge wao, kutoa maoni yao na kushiriki kikamilifu katika kujenga maendeleo ya Jimbo la Kalambo.
RATIBA YA MIKUTANO YA HADHARA
Tarehe: 20 Julai 2026 – 10 Agosti 2026
20/07/2026: Kata ya Samazi – Vijiji vya Kipanga, Katili na Samazi.
21/07/2026: Kata ya Kasanga – Vijiji vya Kipwa na Kapele.
22/07/2026: Kata ya Kasanga na Kisumba – Vijiji vya Kilewani na Kisumba.
23/07/2026: Kata ya Mpomwe – Vijiji vya Nondo, Kapozwa na Mpomwe.
24/07/2026: Kata ya Mkowe – Vijiji vya Limba, Mkowe A na Mkowe B.
25/07/2026: Kata za Mkowe na Lyowa – Vijiji vya Katapulo, Mbuza na Santamaria.
26/07/2026: Kata ya Katazi – Vijiji vya Kafukula, Katazi na Mvula.
27/07/2026: Kata ya Mwazye – Vijiji vya Mpenje, Msoma na Kazila.
28/07/2026: Kata ya Kilesha – Vijiji vya Itekesha, Kambo na Kifone.
29/07/2026: Kata za Lyowa na Msanzi – Vijiji vya Singiwe, Msanzi Kati na Mbuluma.
30/07/2026: Kata za Katete na Sopa – Vijiji vya Jengeni, Kasitu na Mtuntumbe.
31/07/2026: Kata ya Mkali – Vijiji vya Kizombwe, Kalalasi na Myunga.
01/08/2026: Kata ya Katete – Vijiji vya Kaluko, Ngoma na Katete.
02/08/2026: Kata ya Sundu – Vijiji vya Kalaela, Kamawe na Zyangoma.
03/08/2026: Kata ya Mwimbi – Vijiji vya Mozi, Selengoma na Msishindwe.
04/08/2026: Kata ya Kanyezi – Vijiji vya Chalatila, Chisambo na Majengo.
05/08/2026: Kata ya Matai/Nkonswe – Vijiji vya Tunyi, Mzungwa na Kasusu.
06/08/2026: Kata ya Legezamwendo – Vijiji vya Mlenje, Mkombo na Legezamwendo.
10/08/2026: Kata ya Ulumi – Vijiji vya Mnazi, Kale na Ulumi B.
Imetolewa na:
Musa Frackison Mzopola
Katibu wa Mbunge
Jimbo la Kalambo


