📰 HABARI MPYA
Inapakia habari...

🚑 HATIMAYE! UKANDA WA MAMBWE WAPATA GARI LA WAGONJWA; RC CHARLES MAKONGORO NYERERE AFICHUA JINSI MBUNGE KANONI ALIVYOLIFUATILIA HADI KUPATIKANA

  🚑 HATIMAYE! UKANDA WA MAMBWE WAPATA GARI LA WAGONJWA; RC CHARLES MAKONGORO NYERERE AFICHUA JINSI MBUNGE KANONI ALIVYOLIFUATILIA HADI KUPATIKANA

Kalambo, Rukwa | Julai 29, 2026

Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joachim Kanoni, inapenda kuwajulisha wananchi wa Wilaya ya Kalambo kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imekabidhi rasmi gari jipya la wagonjwa kwa ajili ya kuhudumia wananchi wa Ukanda wa Mambwe.

Makabidhiano hayo yalifanyika tarehe 29 Julai, 2026 katika Kata ya Legezamwendo, yakiongozwa na Mhe. Charles Makongoro Nyerere, Mkuu wa Mkoa wa Rukwa. Gari hilo linatarajiwa kuboresha huduma za dharura na kupunguza changamoto za usafirishaji wa wagonjwa katika Ukanda wa Mambwe.

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano, Mhe. Charles Makongoro Nyerere aliwataka wananchi kulitunza gari hilo ili liweze kutoa huduma kwa muda mrefu. Aidha, aliwahimiza wananchi kumshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwajali wananchi wa Kalambo kupitia maboresho makubwa ya huduma za afya.

Kwa upande wa Wilaya ya Kalambo, Mkuu wa Mkoa aliwataka wananchi kumpongeza Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joachim Kanoni, kwa juhudi zake za kuomba na kufuatilia kwa karibu upatikanaji wa gari hilo hadi kufanikisha kupatikana kwake.

Mhe. Charles Makongoro Nyerere alisema kuwa wakati Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Prof. Riziki Silas Shemdoe, alipofanya ziara mkoani Rukwa siku 14 zilizopita, alieleza kuwa Mbunge Kanoni ni mmoja wa wabunge wanaofuatilia kwa karibu mahitaji ya wananchi wao na hakuchoka kuwasilisha maombi serikalini, jambo lililochangia kupatikana kwa gari hilo.











Aidha, Mkuu wa Mkoa alisisitiza kuwa viongozi wanapaswa kuwa na utamaduni wa kufuatilia maendeleo ya wananchi badala ya kusubiri kila jambo lifike kwa utaratibu wa kawaida. Alibainisha kuwa kati ya magari 20 ya wagonjwa yaliyotolewa kwa Tanzania Bara, Mkoa wa Rukwa umefanikiwa kupata magari mawili kutokana na juhudi hizo.

Aliwahimiza pia wananchi kuendelea kushirikiana na Serikali kwa kujenga nyumba za watumishi wa afya ili kuwavutia na kuwawezesha kutoa huduma katika mazingira bora.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joachim Kanoni, alimshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuijali Kalambo kupitia uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya. Vilevile alimshukuru Prof. Riziki Silas Shemdoe, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, pamoja na mawaziri, manaibu mawaziri na watendaji wote wa Serikali kwa ushirikiano walioutoa hadi kufanikisha upatikanaji wa gari hilo.

Mbunge Kanoni aliwahimiza wananchi kulitunza gari hilo ili kiendelee kuwahudumia kwa muda mrefu. Aidha, aliishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuendelea kuimarisha huduma za afya Wilayani Kalambo kupitia utoaji wa shilingi milioni 438 kwa ajili ya ukamilishaji wa Vituo vya Afya vya Legezamwendo, Mwazye na Samazi, pamoja na shilingi milioni 138 kwa ajili ya ukamilishaji wa Kituo cha Afya cha Kanyezi.

Mbunge huyo aliwaomba wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuwa imeendelea kuwajali na kuwathamini. Pia aliwasihi kuendeleza umoja, mshikamano na upendo ili kuharakisha maendeleo ya Wilaya ya Kalambo.

Kwa upande wao, wananchi wa Ukanda wa Mambwe walimshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mbunge Mhe. Edefonsi Joachim Kanoni, pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Mhe. Charles Makongoro Nyerere, kwa kufanikisha upatikanaji wa gari hilo. Kama ishara ya shukrani na kuthamini juhudi hizo, wananchi walimkabidhi Mkuu wa Mkoa mbuzi.


KAZI NA UTU, TUNASONGA MBELE


Imetolewa na:


Musa Frackison Mzopola

Katibu wa Mbunge, Jimbo la Kalambo

MATUKIO KWA NJIA YA PICHA

Inapakia picha...

HABARI MAARUFU

ZIARA YA MHE. KANONI KATIKA JIMBO LA KALAMBO IMEAIRISHWA; HIKI NDICHO KILICHOSABABISHA.

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo na umma kwa ujumla kuwa ziara iliyokuwa imepangwa kufanyika kuanzia tarehe 20 Julai 2026 hadi tarehe 10 Agosti 2026 imeahirishwa. Uamuzi huo umetokana na zuio la Serikali kuhusu kufanyika kwa mikutano ya hadhara katika kipindi hiki. Ofisi ya Mbunge inaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza na inaendelea kuwashukuru wananchi kwa ushirikiano na uelewa wao. Kwa taarifa zaidi na maendeleo ya shughuli za Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, tembelea: www.mbungekalambo.com Imetolewa na: Musa Frackison Mzopola Katibu wa Mbunge, Jimbo la Kalambo

HATIMAYE! ORODHA RASMI YA WANUFAIKA WA MIKOPO YA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI KWA WILAYA YA KALAMBO YATOLEWA – WANUFAIKA WOTE WATAKIWA KUHUDHURIA MAFUNZO MUHIMU

  TAARIFA KWA UMMA Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwajulisha wananchi wote wa Wilaya ya Kalambo kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekamilisha mapitio ya maombi ya mikopo yaliyowasilishwa na wananchi wa Wilaya ya Kalambo kupitia programu ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi. Kutokana na mchakato huo, Wizara imetoa rasmi orodha ya wanufaika waliokidhi vigezo na kufanikiwa kupata mikopo hiyo. Wanufaika kutoka Wilaya ya Kalambo ni kama ilivyoainishwa katika orodha rasmi ya Wizara, ambayo inajumuisha: Rahel John Mawela – Mradi wa Mbuzi Faustina Cladio Msumeno – Mradi wa Kuku wa Mayai William Isaya Moringe – Mradi wa Mbuzi Mashaka Medard Jastin – Mradi wa Mfumo wa Ubaridi Aibini Leonard John – Mradi wa Mbuzi Britney Shadi Pandisha – Mradi wa Kuku wa Nyama Sisilia Augustino Michael – Mradi wa Mbuzi Ofisi ya Mbunge inawapongeza wanufaika wote kwa kufanikiwa kupata fursa hiyo muhimu na inawatakia mafanikio katika utekelezaji wa ...

ZIARA YA MIKUTANO YA HADHARA YA MHE. EDEFONSI JOACKIM KANONI MBUNGE JIMBO LA KALAMBO YATANGAZWA

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo kuwa Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni (Mb), Mbunge wa Jimbo la Kalambo, atafanya ziara ya mikutano ya hadhara katika kata na vijiji mbalimbali vya jimbo kuanzia tarehe 20 Julai, 2026 hadi tarehe 10 Agosti, 2026, kwa mujibu wa ratiba iliyoambatanishwa.    Ziara hii inalenga kuimarisha mawasiliano kati ya Mbunge na wananchi kwa kukutana nao ana kwa ana, kusikiliza maoni, kero na changamoto zinazowakabili, pamoja na kupokea mapendekezo yatakayosaidia kuboresha huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo ya Jimbo la Kalambo. Aidha, Mhe. Mbunge atatoa mrejesho kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kueleza mipango ya maendeleo inayotarajiwa kutekelezwa katika maeneo mbalimbali ya jimbo. Wananchi watapata fursa ya kuuliza maswali, kutoa maoni yao na kushiriki katika kujadili masuala muhimu yanayohusu maendeleo ya kata na vijiji vyao. Ushiriki wa wananchi katika mikutano hii ni msingi m...