KALAMBO: Katika kipindi cha uongozi wake, Mhe. Edefonce Joackim Kanoni, Mbunge wa Jimbo la Kalambo, ameendelea kuweka msukumo katika kuboresha sekta ya elimu kwa kuwasilisha changamoto za wananchi Serikalini na kufuatilia upatikanaji wa fedha kwa ajili ya miundombinu ya shule.
Miongoni mwa mambo makubwa yaliyofanyika ni ufuatiliaji wa umaliziaji wa magofu 143 ya vyumba vya madarasa, hatua inayolenga kuongeza nafasi za kujifunzia na kuboresha mazingira ya elimu katika maeneo mbalimbali ya Jimbo la Kalambo.
Kupitia Mfuko wa Jimbo, kiasi cha shilingi milioni 173 kilipatikana na kutumika katika miradi mbalimbali ya maendeleo, ambapo sehemu ya fedha hizo ilitumika katika umaliziaji wa vyumba 20 vya madarasa.
Aidha, Serikali imeingiza shilingi milioni 580 kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Sekondari Kanyezi, ikiwa ni hatua muhimu katika kuongeza miundombinu ya elimu na kuwasaidia wanafunzi kupata huduma ya elimu katika mazingira bora.
Mhe. Kanoni pia amewasilisha na kufuatilia ombi la ujenzi wa shule tatu za sekondari katika kata ya Kilesha Sundu na Lyowa ambazo bado hazina shule za sekondari, akisisitiza umuhimu wa kuhakikisha wanafunzi wanapata fursa ya kuendelea na elimu ya sekondari bila kulazimika kusafiri umbali mrefu.
Juhudi hizo zinaelezwa kuwa sehemu ya utekelezaji wa wajibu wa Mbunge wa kuwakilisha wananchi, kuwasilisha changamoto zao na kufuatilia hatua za Serikali katika kutatua changamoto za sekta ya elimu.
Kwa ujumla, hatua hizo zinaonyesha msukumo unaowekwa katika kuongeza miundombinu ya elimu, kupunguza changamoto ya vyumba vya madarasa na kuongeza upatikanaji wa shule za sekondari katika Jimbo la Kalambo.
ELIMU BORA, MSINGI WA MAENDELEO YA KALAMBO.
Imetolewa na:
Musa Frackison Mzopola
Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Kalambo


💬 Toa Maoni Kuhusu Habari Hii
Umemaliza kusoma habari hii? Tupe maoni, mtazamo au swali lako hapa chini.
Comments
Post a Comment