Dodoma: Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni, inampongeza Mhe. Deogratius Ndejembi kwa kuthibitishwa na Bunge kuwa Makamu wa Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mhe. Ndejembi amethibitishwa baada ya kupata kura 324 za “Ndiyo” kutoka kwa Wabunge katika mchakato uliofanyika leo, Agosti 28, 2026, katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Dodoma.
Ofisi ya Mbunge Jimbo la Kalambo inatoa pongezi za dhati kwa Mhe. Deogratius Ndejembi kwa hatua hiyo muhimu ya kitaifa, huku ikimtakiwa hekima, busara, uadilifu na mafanikio katika kutekeleza majukumu yake mapya kwa manufaa ya Taifa na wananchi wake.
Aidha, Ofisi ya Mbunge Jimbo la Kalambo inaamini kuwa Mhe. Ndejembi ataendelea kutumia nafasi hiyo katika kuimarisha umoja, mshikamano, amani na maendeleo ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akizingatia maslahi ya Watanzania wote.
Ofisi ya Mbunge Jimbo la Kalambo inamtakia Mhe. Deogratius Ndejembi kila la heri katika hatua hii mpya ya utumishi wa Taifa na katika utekelezaji wa majukumu yake ya kitaifa.
IMETOLEWA NA:
MUSA FRACKISON MZOPOLA
KATIBU WA MBUNGE JIMBO LA KALAMBO


💬 Toa Maoni Kuhusu Habari Hii
Umemaliza kusoma habari hii? Tupe maoni, mtazamo au swali lako hapa chini.
Comments
Post a Comment