📰 HABARI MPYA
Inapakia habari...

SERIKALI YA AWAMU YA SITA YAENDELEA KUIMARISHA HUDUMA ZA AFYA KALAMBO KWA KUTENGA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 1.2

SERIKALI YA AWAMU YA SITA YAENDELEA KUIMARISHA HUDUMA ZA AFYA KALAMBO KWA KUTENGA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 1.2

 

Ofisi ya Mbunge Jimbo la Kalambo inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuonesha dhamira ya dhati ya kuboresha huduma za afya kwa kutenga zaidi ya shilingi bilioni 1.2 kwa ajili ya ujenzi na ukamilishaji wa vituo vya afya na zahanati mbalimbali ndani ya Jimbo la Kalambo.

Akizungumza wakati wa kukabidhi gari la wagonjwa (Ambulance) katika Kata ya Legezamwendo, Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni, amesema kuwa uwekezaji huo unaonesha wazi jinsi Serikali inavyoweka kipaumbele katika kuimarisha sekta ya afya kwa kusogeza huduma karibu na wananchi ili kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora, salama na kwa wakati. Amesema dhamira ya Serikali ni kuendelea kuboresha afya za wananchi, kupunguza vifo vinavyoweza kuzuilika, kuimarisha huduma za afya ya mama na mtoto, pamoja na kuongeza ustawi wa jamii kupitia huduma bora za matibabu.

Mhe. Kanoni amesema kuwa katika utekelezaji wa mpango huo, Serikali imetenga shilingi milioni 650 kupitia Serikali Kuu kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Ulumi, shilingi milioni 300 kwa ajili ya umaliziaji wa Vituo vya Afya Mwazye na Legezamwendo, shilingi milioni 60 kutoka mapato ya Halmashauri kwa ajili ya umaliziaji wa Kituo cha Afya Samazi, shilingi milioni 138 kwa ajili ya umaliziaji wa Kituo cha Afya Kanyezi, pamoja na shilingi milioni 106 kwa ajili ya umaliziaji wa Zahanati ya Kijiji cha Tunyi, Kata ya Mambwenkoswe.

Amesema kukamilika kwa miradi hiyo kutapunguza adha ya wananchi kusafiri umbali mrefu kutafuta huduma za matibabu, kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto, kuongeza uwezo wa kuhudumia wagonjwa wa dharura, kuimarisha mazingira ya kazi kwa watumishi wa afya na kuongeza upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wananchi wote. Aidha, amesema uwekezaji huo utachochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa kuwa wananchi wenye afya njema hushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji na maendeleo ya Taifa.

Mbunge huyo ameishukuru kwa dhati Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuendelea kupeleka fedha za maendeleo katika Jimbo la Kalambo. Pia ametoa shukrani kwa Mawaziri, Manaibu Mawaziri, viongozi wa Mkoa wa Rukwa, Wilaya ya Kalambo pamoja na watendaji wote wa Serikali kwa ushirikiano mkubwa wanaouonesha katika kuhakikisha miradi ya maendeleo inatekelezwa na kuwanufaisha wananchi.

Aidha, Mhe. Kanoni amewaomba wananchi wa Jimbo la Kalambo kuendelea kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi hiyo ili fedha zilizotengwa zitumike kwa uadilifu, uwazi na ufanisi. Amesisitiza kuwa fedha hizo ni mali ya wananchi zinazotokana na kodi zao, hivyo kila mwananchi ana wajibu wa kuzilinda na kuhakikisha miradi inakamilika kwa viwango vinavyokusudiwa.

Katika hitimisho la hotuba yake, Mhe. Kanoni ametoa wito kwa wananchi kuendelea kudumisha upendo, amani, umoja na mshikamano, akieleza kuwa misingi hiyo ndiyo nguzo muhimu ya maendeleo endelevu. Amesema kwa kuendelea kushirikiana na kuiunga mkono Serikali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, Jimbo la Kalambo litaendelea kupiga hatua kubwa za maendeleo.

KAZI NA UTU, TUNASONGA MBELE.

Imetolewa na:
Musa Frackison Mzopola
Katibu wa Mbunge Jimbo la Kalambo

MATUKIO KWA NJIA YA PICHA

Inapakia picha...

HABARI MAARUFU

ZIARA YA MHE. KANONI KATIKA JIMBO LA KALAMBO IMEAIRISHWA; HIKI NDICHO KILICHOSABABISHA.

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo na umma kwa ujumla kuwa ziara iliyokuwa imepangwa kufanyika kuanzia tarehe 20 Julai 2026 hadi tarehe 10 Agosti 2026 imeahirishwa. Uamuzi huo umetokana na zuio la Serikali kuhusu kufanyika kwa mikutano ya hadhara katika kipindi hiki. Ofisi ya Mbunge inaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza na inaendelea kuwashukuru wananchi kwa ushirikiano na uelewa wao. Kwa taarifa zaidi na maendeleo ya shughuli za Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, tembelea: www.mbungekalambo.com Imetolewa na: Musa Frackison Mzopola Katibu wa Mbunge, Jimbo la Kalambo

HATIMAYE! ORODHA RASMI YA WANUFAIKA WA MIKOPO YA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI KWA WILAYA YA KALAMBO YATOLEWA – WANUFAIKA WOTE WATAKIWA KUHUDHURIA MAFUNZO MUHIMU

  TAARIFA KWA UMMA Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , inapenda kuwajulisha wananchi wote wa Wilaya ya Kalambo kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekamilisha mapitio ya maombi ya mikopo yaliyowasilishwa na wananchi wa Wilaya ya Kalambo kupitia programu ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi. Kutokana na mchakato huo, Wizara imetoa rasmi orodha ya wanufaika waliokidhi vigezo na kufanikiwa kupata mikopo hiyo. Wanufaika kutoka Wilaya ya Kalambo ni kama ilivyoainishwa katika orodha rasmi ya Wizara, ambayo inajumuisha: Rahel John Mawela – Mradi wa Mbuzi Faustina Cladio Msumeno – Mradi wa Kuku wa Mayai William Isaya Moringe – Mradi wa Mbuzi Mashaka Medard Jastin – Mradi wa Mfumo wa Ubaridi Aibini Leonard John – Mradi wa Mbuzi Britney Shadi Pandisha – Mradi wa Kuku wa Nyama Sisilia Augustino Michael – Mradi wa Mbuzi Ofisi ya Mbunge inawapongeza wanufaika wote kwa kufanikiwa kupata fursa hiyo muhimu na inawatakia mafanikio katika utekelezaji wa ...

ZIARA YA MIKUTANO YA HADHARA YA MHE. EDEFONSI JOACKIM KANONI MBUNGE JIMBO LA KALAMBO YATANGAZWA

  Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kalambo inapenda kuwataarifu wananchi wote wa Jimbo la Kalambo kuwa Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni (Mb), Mbunge wa Jimbo la Kalambo, atafanya ziara ya mikutano ya hadhara katika kata na vijiji mbalimbali vya jimbo kuanzia tarehe 20 Julai, 2026 hadi tarehe 10 Agosti, 2026, kwa mujibu wa ratiba iliyoambatanishwa.    Ziara hii inalenga kuimarisha mawasiliano kati ya Mbunge na wananchi kwa kukutana nao ana kwa ana, kusikiliza maoni, kero na changamoto zinazowakabili, pamoja na kupokea mapendekezo yatakayosaidia kuboresha huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo ya Jimbo la Kalambo. Aidha, Mhe. Mbunge atatoa mrejesho kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kueleza mipango ya maendeleo inayotarajiwa kutekelezwa katika maeneo mbalimbali ya jimbo. Wananchi watapata fursa ya kuuliza maswali, kutoa maoni yao na kushiriki katika kujadili masuala muhimu yanayohusu maendeleo ya kata na vijiji vyao. Ushiriki wa wananchi katika mikutano hii ni msingi m...