Mhe. Edifonsi Joackim Kanoni, Mbunge wa Jimbo la Kalambo, anaendelea ahadi aliyoitoa kwa wananchi wakati wa kampeni za uchaguzi kwa maamuzi na dira ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia Ilani ya Uchaguzi wa mwaka 2025–2030, ambayo inalenga kuwa na vitongoji vyote 422 vya Jimbo la Kalambo vinafikiwa na huduma ya umeme ifikapo mwaka 2030.
Katika miezi sita tangu aanze kutekeleza majukumu yake kama Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Kanoni ameendelea kupambania maendeleo ya wananchi wake kwa vitendo. Kupitia juhudi zake za karibu na Serikali pamoja na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), vitongoji 35 tayari vimeidhinishwa kuunganishwa na huduma umeme ambapo mkataba umeshasainiwa, upembuzi yakinifu umekamilika na kazi ya kusambaza nguzo imeanza rasmi.
Hatua hii ni sehemu ya utekelezaji wa mpango mkubwa wa kusaidia wananchi wote wa Kalambo wanapata huduma ya umeme kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Kwa sasa vimebakia vitongoji 28 ili kukamilisha awamu ya utekelezaji.
Mhe. Kanoni amewaomba wananchi maeneo ambayo bado hayajafikiwa na huduma ya umeme kuwa na subira, akieleza miradi ya REA kutekeleza na mipango na upatikanaji wa rasilimali. Amesisitiza kuwa vitongoji vyote vilivyobaki vitafikiwa kwa mujibu wa ratiba ya Serikali.
Aidha, Mbunge huyo ameipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na Mawaziri, viongozi na watendaji mbalimbali wa Serikali kwa wanaompatia maendeleo yanafika kwa wananchi wa Kalambo na Watanzania kwa ujumla.
Amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuonesha kuwa ni serikali sikivu, inayojali na kuthamini maisha ya Watanzania kwa kupeleka huduma muhimu za maendeleo hadi ngazi ya wananchi wa kawaida.
Mhe. Kanoni amewasihi wananchi wa Kalambo kuendelea kuiamini Serikali yao, kuunga mkono juhudi za maendeleo zinazotekelezwa na umoja, mshikamano na utu, akisisitiza ndiyo msingi wa maendeleo.
Orodha ya Vitongoji Vilivyopangwa Kufikiwa na Umeme katika Awamu Hii
Nchenje – Kijiji Utengule, Kata Mambwenkowe
Mombokaku – Kijiji Mombo, Kata Legezamwendo
Kawala – Kijiji Kanyalakata, Kata Mbuluma
Uhuru – Kijiji Mlenje, Kata Legezamwendo
Nchese – Kijiji Kachele, Kata Kisumba
Kavusha – Kijiji Kileweli, Kata Kasanga
Kantundulu – Kijiji Kalembe, Kata Mambwenkowe
Molwe – Kijiji Muzi, Kata Kasanga
Kalepa – Kijiji Kisala, Kata Samazi
Mkwavi – Kijiji Kisala, Kata Samazi
Namkonda – Kijiji Chipapa, Kata Mwimbi
Mkombo – Kijiji Mkombo, Kata Legezamwendo
Fena – Kijiji Kalepula “A”, Kata Ulumi
Kasamvu – Kijiji Mikonko, Kata Matai
Katindizi – Kijiji Mpombwe, Kata Mpombwe
Iyala – Kijiji Chipapa, Kata Mwimbi
Mizumbi – Kijiji Itekesha, Kata Kilesha
Kamisuku – Kijiji Kanyezi, Kata Kanyezi
Mchenje – Kijiji Kantalemwa, Kata Mnamba
Chaptuka – Kijiji Kapozwa, Kata Mpombwe
Mwela – Kijiji Safu, Kata Katete
Mlembuke/Kapewa – Kijiji Sopa, Kata Sopa
Wala – Kijiji Katazi, Kata Katazi
Mipapa – Kijiji Msipazi, Kata Mnamba
Makale – Kijiji Kaluko, Kata Katete
Vitongoji vinavyo Subiri Kuhidhinishwa na kuingia kwenye Mpango wa Utekelezaji
Kamatwa – Kijiji Katuka, Kata Msanzi
Munwa – Kijiji Limba, Kata Mkowe
Kanamwene – Kijiji Mzungu, Kata Kalembe
Lolesha – Kijiji Madibila, Kata Mambwenkowe
Mbita – Kijiji Kipampa, Kata Samazi
Isale – Kijiji Madibila, Kata Mambwenkowe
Miakasi – Kijiji Kisala, Kata Samazi
Mbangizya – Kijiji Mtutumbe, Kata Sopa
Kalemasha – Kijiji Lolesha, Kata Mbuluma
Kamisuku – Kijiji Mpanga, Kata Mambwenkowe
“Umoja, Mshikamano na Utu ndiyo nguzo ya maendeleo.”

