📰 HABARI MPYA
Inapakia habari...

MBUNGE WA JIMBO LA KALAMBO MHE. EDIFONSI KANONI AENDELEA KUTEKELEZA AHADI YA UMEME KWA VITONGOJI VYOTE VYA JIMBO LA KALAMBO

MBUNGE WA JIMBO LA KALAMBO MHE. EDIFONSI KANONI AENDELEA KUTEKELEZA AHADI YA UMEME KWA VITONGOJI VYOTE VYA JIMBO LA KALAMBO

 


Mhe. Edifonsi Joackim Kanoni, Mbunge wa Jimbo la Kalambo, anaendelea ahadi aliyoitoa kwa wananchi wakati wa kampeni za uchaguzi kwa maamuzi na dira ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia Ilani ya Uchaguzi wa mwaka 2025–2030, ambayo inalenga kuwa na vitongoji vyote 422 vya Jimbo la Kalambo vinafikiwa na huduma ya umeme ifikapo mwaka 2030.

Katika miezi sita tangu aanze kutekeleza majukumu yake kama Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Kanoni ameendelea kupambania maendeleo ya wananchi wake kwa vitendo. Kupitia juhudi zake za karibu na Serikali pamoja na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), vitongoji 35 tayari vimeidhinishwa kuunganishwa na huduma umeme ambapo mkataba umeshasainiwa, upembuzi yakinifu umekamilika na kazi ya kusambaza nguzo imeanza rasmi.

Hatua hii ni sehemu ya utekelezaji wa mpango mkubwa wa kusaidia wananchi wote wa Kalambo wanapata huduma ya umeme kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Kwa sasa vimebakia vitongoji 28 ili kukamilisha awamu ya utekelezaji.

Mhe. Kanoni amewaomba wananchi maeneo ambayo bado hayajafikiwa na huduma ya umeme kuwa na subira, akieleza miradi ya REA kutekeleza na mipango na upatikanaji wa rasilimali. Amesisitiza kuwa vitongoji vyote vilivyobaki vitafikiwa kwa mujibu wa ratiba ya Serikali.

Aidha, Mbunge huyo ameipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na Mawaziri, viongozi na watendaji mbalimbali wa Serikali kwa wanaompatia maendeleo yanafika kwa wananchi wa Kalambo na Watanzania kwa ujumla.

Amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuonesha kuwa ni serikali sikivu, inayojali na kuthamini maisha ya Watanzania kwa kupeleka huduma muhimu za maendeleo hadi ngazi ya wananchi wa kawaida.

Mhe. Kanoni amewasihi wananchi wa Kalambo kuendelea kuiamini Serikali yao, kuunga mkono juhudi za maendeleo zinazotekelezwa na umoja, mshikamano na utu, akisisitiza ndiyo msingi wa maendeleo.

Orodha ya Vitongoji Vilivyopangwa Kufikiwa na Umeme katika Awamu Hii

  1. Nchenje – Kijiji Utengule, Kata Mambwenkowe

  2. Mombokaku – Kijiji Mombo, Kata Legezamwendo

  3. Kawala – Kijiji Kanyalakata, Kata Mbuluma

  4. Uhuru – Kijiji Mlenje, Kata Legezamwendo

  5. Nchese – Kijiji Kachele, Kata Kisumba

  6. Kavusha – Kijiji Kileweli, Kata Kasanga

  7. Kantundulu – Kijiji Kalembe, Kata Mambwenkowe

  8. Molwe – Kijiji Muzi, Kata Kasanga

  9. Kalepa – Kijiji Kisala, Kata Samazi

  10. Mkwavi – Kijiji Kisala, Kata Samazi

  11. Namkonda – Kijiji Chipapa, Kata Mwimbi

  12. Mkombo – Kijiji Mkombo, Kata Legezamwendo

  13. Fena – Kijiji Kalepula “A”, Kata Ulumi

  14. Kasamvu – Kijiji Mikonko, Kata Matai

  15. Katindizi – Kijiji Mpombwe, Kata Mpombwe

  16. Iyala – Kijiji Chipapa, Kata Mwimbi

  17. Mizumbi – Kijiji Itekesha, Kata Kilesha

  18. Kamisuku – Kijiji Kanyezi, Kata Kanyezi

  19. Mchenje – Kijiji Kantalemwa, Kata Mnamba

  20. Chaptuka – Kijiji Kapozwa, Kata Mpombwe

  21. Mwela – Kijiji Safu, Kata Katete

  22. Mlembuke/Kapewa – Kijiji Sopa, Kata Sopa

  23. Wala – Kijiji Katazi, Kata Katazi

  24. Mipapa – Kijiji Msipazi, Kata Mnamba

  25. Makale – Kijiji Kaluko, Kata Katete

Vitongoji vinavyo Subiri Kuhidhinishwa na kuingia kwenye Mpango wa Utekelezaji

  1. Kamatwa – Kijiji Katuka, Kata Msanzi

  2. Munwa – Kijiji Limba, Kata Mkowe

  3. Kanamwene – Kijiji Mzungu, Kata Kalembe

  4. Lolesha – Kijiji Madibila, Kata Mambwenkowe

  5. Mbita – Kijiji Kipampa, Kata Samazi

  6. Isale – Kijiji Madibila, Kata Mambwenkowe

  7. Miakasi – Kijiji Kisala, Kata Samazi

  8. Mbangizya – Kijiji Mtutumbe, Kata Sopa

  9. Kalemasha – Kijiji Lolesha, Kata Mbuluma

  10. Kamisuku – Kijiji Mpanga, Kata Mambwenkowe

“Umoja, Mshikamano na Utu ndiyo nguzo ya maendeleo.”

KAZI NA UTU, TUNASONGA MBELE

Imetolewa na:
Musa Frackison Mzopola
Katibu wa Mbunge, Jimbo la Kalambo .


Umemaliza kusoma habari hii? Tupe maoni, mtazamo au swali lako hapa chini.

Comments

Post a Comment

MATUKIO KWA NJIA YA PICHA

Inapakia picha...

HABARI MAARUFU

FURSA ZA MIKOPO YA VIJANA SASA HADHARANI OMBA SASA UJIKWAMUE KIUCHUMI

  Katika kutekeleza ahadi ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya kutoa shilingi bilioni 200 kwa vijana ndani ya siku 100 baada ya kuingia madarakani, Wizara ya Mifugo na Uvuvi inautangazia umma kuanza kwa Awamu ya Pili ya utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu kwa vijana. Malengo ya mikopo hiyo ni kuwawezesha vijana kupata mitaji ya kuanzisha na kuendeleza biashara ndogo, biashara za kati na kampuni changa ili kujijengea kipato katika Sekta za Mifugo na Uvuvi. Mikopo hiyo itatolewa kwa njia ya vifaa na pembejeo za uzalishaji, ikiwemo ufugaji wa samaki kwa vizimba, ufugaji wa kuku (chotara, mayai na nyama), mbuzi, kondoo na nguruwe, pamoja na boti za kuhudumia vizimba, boti za uvuvi, zana za uvuvi, mifumo ya ubari (cold chain) katika mazao ya uvuvi, mifumo ya kulazisha vifaranga vya samaki, mifumo na vifaa vya uchakataji wa mazao ya uvuvi ikijumuisha makausho ya dagaa na mwani (dryers). Vigezo na maelekezo kwa waombaji ni kama ifuatavyo: i. Baru...

NAFASI 200 ZA AJIRA ZA MAFUNDI ZATANGAZWA KWA KAZI NCHINI SAUDI ARABIA

  Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, kwa kushirikiana na Atilis Investment Limited , inawataarifu Watanzania wenye sifa stahiki kuhusu nafasi 200 za ajira za mafundi katika sekta ya ujenzi , zilizotolewa na kampuni ya Shade Corporation Limited ya nchini Saudi Arabia. KADA ZINAZOHITAJIKA Nafasi hizo zinahusisha mafundi wa kada mbalimbali, wakiwemo: Mafundi Uashi Mafundi Useremala Wasuka Nondo SIFA ZA MWOMBAJI Mwombaji anatakiwa kuwa na: Elimu ya astashahada kutoka chuo cha ufundi kinachotambuliwa na Serikali; Uzoefu wa kazi wa miaka miwili (2) au zaidi katika sekta ya ufundi; Uwezo na uzoefu katika kada husika, ikiwemo Uashi, Useremala au Usuka Nondo; Umri kati ya miaka 21 hadi 40 ; Waombaji wa nafasi hizi wanatakiwa kuwa wanaume . MASHARTI NA MAFANO YA AJIRA Waombaji watakaofaulu mchakato wa ajira watapata fursa ya kufanya kazi nchini Saudi Arabia kwa masharti yaliyowekwa na mwajiri. Miongoni mwa mafao na masharti ya ajira ni: Mshahara wa Riyal 1...

MHE. MBUNGE KANONI ASHIRIKI MAZISHI YA WAATHIRIKA WA AJALI KAZILA, ATOA WITO WA UPENDO, UMOJA NA MSHIKAMANO

  KALAMBO: Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , ameshiriki mazishi ya wananchi wawili waliofariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea katika Kijiji cha Kazila, Kata ya Mwazye, Wilaya ya Kalambo, huku akitoa pole na faraja kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki pamoja na wananchi wote walioguswa na msiba huo. Ajali hiyo ilitokea tarehe 05 Agosti 2026 , wakati gari aina ya Fuso lililokuwa limebeba watu waliokuwa wakielekea kwenye shughuli ya harusi kutoka Kijiji cha Msoma, Kata ya Mwazye, Wilaya ya Kalambo , lilipofika katika Kijiji cha Kazila kwa ajili ya shughuli ya kufunga ndoa. Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa, gari hilo lilikuwa limembeba bwana harusi, Hosea Gilbert Watua , pamoja na watu wengine waliokuwa wakisafiri naye kutoka Kijiji cha Msoma kuelekea Kijiji cha Kazila, ambako alikuwa akienda kufunga ndoa na bibi harusi, Mehili Sauli Visent , mkazi wa Kijiji cha Kazila, Kata ya Mwazye. AJALI YATOKEA KABLA YA KUFIKA KWENYE DARAJA Taarifa zinaeleza ...