📰 HABARI MPYA
Inapakia habari...

MHE. EDIFONSI KANONI ATEULIWA KUWA MJUMBE WA CHAMA CHA KIRAFIKI KATI YA BUNGE LA TANZANIA NA BUNGE LA INDIA

MHE. EDIFONSI KANONI ATEULIWA KUWA MJUMBE WA CHAMA CHA KIRAFIKI KATI YA BUNGE LA TANZANIA NA BUNGE LA INDIA

 


Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edifonsi Joackim Kanoni, ameteuliwa rasmi kuwa mmoja wa wajumbe 10 wanaounda Chama cha Kirafiki cha Kibunge kati ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Bunge la India.

Kwa mujibu wa barua ya Katibu wa Bunge yenye kumbukumbu namba QA.203/261/01/48 ya tarehe 15 Juni 2026, uteuzi huo umefanywa na Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mb), kwa lengo la kuimarisha ushirikiano, urafiki na diplomasia ya kibunge kati ya Tanzania na India.

Chama hicho kinaundwa na wabunge 10 walioteuliwa kutoka Bunge la Tanzania kwa ajili ya kushiriki shughuli mbalimbali za kuendeleza mahusiano ya kirafiki na kubadilishana uzoefu katika sekta mbalimbali za maendeleo kati ya nchi hizo mbili.

Aidha, Balozi wa India nchini Tanzania anatarajiwa kukutana na kufanya mazungumzo na wajumbe wa chama hicho tarehe 24 au 25 Juni 2026 katika Ofisi za Bunge jijini Dodoma, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha ushirikiano kati ya mabunge ya nchi hizo mbili.

Uteuzi wa Mhe. Kanoni ni heshima kubwa kwa Jimbo la Kalambo, Mkoa wa Rukwa na Taifa kwa ujumla, ukiwa ni ishara ya imani kubwa aliyopewa katika kuwakilisha Tanzania kwenye masuala ya ushirikiano wa kimataifa kupitia diplomasia ya kibunge.

Imetolewa

Musa Frackison Mzopola

Katibu wa Mbunge jimbo la Kalambo

Umemaliza kusoma habari hii? Tupe maoni, mtazamo au swali lako hapa chini.

Comments

Post a Comment

MATUKIO KWA NJIA YA PICHA

Inapakia picha...

HABARI MAARUFU

FURSA ZA MIKOPO YA VIJANA SASA HADHARANI OMBA SASA UJIKWAMUE KIUCHUMI

  Katika kutekeleza ahadi ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya kutoa shilingi bilioni 200 kwa vijana ndani ya siku 100 baada ya kuingia madarakani, Wizara ya Mifugo na Uvuvi inautangazia umma kuanza kwa Awamu ya Pili ya utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu kwa vijana. Malengo ya mikopo hiyo ni kuwawezesha vijana kupata mitaji ya kuanzisha na kuendeleza biashara ndogo, biashara za kati na kampuni changa ili kujijengea kipato katika Sekta za Mifugo na Uvuvi. Mikopo hiyo itatolewa kwa njia ya vifaa na pembejeo za uzalishaji, ikiwemo ufugaji wa samaki kwa vizimba, ufugaji wa kuku (chotara, mayai na nyama), mbuzi, kondoo na nguruwe, pamoja na boti za kuhudumia vizimba, boti za uvuvi, zana za uvuvi, mifumo ya ubari (cold chain) katika mazao ya uvuvi, mifumo ya kulazisha vifaranga vya samaki, mifumo na vifaa vya uchakataji wa mazao ya uvuvi ikijumuisha makausho ya dagaa na mwani (dryers). Vigezo na maelekezo kwa waombaji ni kama ifuatavyo: i. Baru...

NAFASI 200 ZA AJIRA ZA MAFUNDI ZATANGAZWA KWA KAZI NCHINI SAUDI ARABIA

  Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, kwa kushirikiana na Atilis Investment Limited , inawataarifu Watanzania wenye sifa stahiki kuhusu nafasi 200 za ajira za mafundi katika sekta ya ujenzi , zilizotolewa na kampuni ya Shade Corporation Limited ya nchini Saudi Arabia. KADA ZINAZOHITAJIKA Nafasi hizo zinahusisha mafundi wa kada mbalimbali, wakiwemo: Mafundi Uashi Mafundi Useremala Wasuka Nondo SIFA ZA MWOMBAJI Mwombaji anatakiwa kuwa na: Elimu ya astashahada kutoka chuo cha ufundi kinachotambuliwa na Serikali; Uzoefu wa kazi wa miaka miwili (2) au zaidi katika sekta ya ufundi; Uwezo na uzoefu katika kada husika, ikiwemo Uashi, Useremala au Usuka Nondo; Umri kati ya miaka 21 hadi 40 ; Waombaji wa nafasi hizi wanatakiwa kuwa wanaume . MASHARTI NA MAFANO YA AJIRA Waombaji watakaofaulu mchakato wa ajira watapata fursa ya kufanya kazi nchini Saudi Arabia kwa masharti yaliyowekwa na mwajiri. Miongoni mwa mafao na masharti ya ajira ni: Mshahara wa Riyal 1...

MHE. MBUNGE KANONI ASHIRIKI MAZISHI YA WAATHIRIKA WA AJALI KAZILA, ATOA WITO WA UPENDO, UMOJA NA MSHIKAMANO

  KALAMBO: Mbunge wa Jimbo la Kalambo, Mhe. Edefonsi Joackim Kanoni , ameshiriki mazishi ya wananchi wawili waliofariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea katika Kijiji cha Kazila, Kata ya Mwazye, Wilaya ya Kalambo, huku akitoa pole na faraja kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki pamoja na wananchi wote walioguswa na msiba huo. Ajali hiyo ilitokea tarehe 05 Agosti 2026 , wakati gari aina ya Fuso lililokuwa limebeba watu waliokuwa wakielekea kwenye shughuli ya harusi kutoka Kijiji cha Msoma, Kata ya Mwazye, Wilaya ya Kalambo , lilipofika katika Kijiji cha Kazila kwa ajili ya shughuli ya kufunga ndoa. Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa, gari hilo lilikuwa limembeba bwana harusi, Hosea Gilbert Watua , pamoja na watu wengine waliokuwa wakisafiri naye kutoka Kijiji cha Msoma kuelekea Kijiji cha Kazila, ambako alikuwa akienda kufunga ndoa na bibi harusi, Mehili Sauli Visent , mkazi wa Kijiji cha Kazila, Kata ya Mwazye. AJALI YATOKEA KABLA YA KUFIKA KWENYE DARAJA Taarifa zinaeleza ...